Friday, September 28, 2012

homa ya watani wa jadi

wakati mchezo kati ya watani wa jadi tanzania simba na yanga ikizidi kupanda mashabiki wa timu hizo mbili wameendelea kutambiana kabla ya mchezo huo.baadhi ya mashabiki wa mchezo hao wamedai kuwa timu zote zimesajili kwa umakini mkubwa na kilichobaki ni mbinu mbali mbali za uwanjani.watani hao watakutana jumatano ijayo ya tarehe 3 katika uwanja wa taifa jijijini dar es salaam

Tuesday, September 25, 2012

Tanzania kuongoza kikosi cha Jeshi la Kimataifa DRC

Tanzania imepewa jukumu la kusimamia na kuongoza kikosi cha jeshi la kimataifa la nchi za maziwa makuu lisiloegemea upande wowote litakalokuwa Mpakani mwa DRC na Rwanda.Hii ina tafsiri gani kwa jeshi letu na nchi yetu? Je ila Sifa ya JWTZ iliyojengwa na Mwalimu kipindi kile bado ipo hadi leo au haya mataifa yanaendelea kuamini hivyo wakati sio kweli? Au ni kweli Jeshi letu bado lipo makini na madhubuti hasa ukizingatia bado linashiriki katika operesheni nyingi za kulinda amani kimataifa?
[caption id="attachment_38" align="alignleft" width="300"] MTOTO WA WAZIRI STEVEN WASIRA AKIJIUNGA NA CHAMA CHA DEMOCRASIA NA MAENDELEO CHADEMA KATIKA TAWI LAKE LILILOPO HUKO MAREKANI[/caption]

kizazi kipyaa

[caption id="attachment_21" align="aligncenter" width="300"] MSANII WA MUZIKI WA KIZAZI KIPYA NCHINI TANZANIA BIBI CHEKA AKIKATIKA NA MSANII MDOGO DOGO ASLAY KATIKA MOJA YA MITAMASHA YAO[/caption]

Monday, September 24, 2012

CCM yapasuka? Kinana ang'atuka...

Mjumbe wa Almashauri kuu na kamati kuu ya CCM captain Abdulharaman kianana amejiuzulu nafasi zota alizonazo ndani ya CCM kwa madai ya kuachana na siasa uchwara.

Kinana amekuwa mjumbe wa NEC kwa zaidi ya miaka 22 pia amewahi kuwa waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga taifa.

Jumatano ndio mambo yote, baada ya NEC huenda viongozi wengi wa CCM wakahamia upinzani.

Tuesday, September 18, 2012

Mh. Pinda alazimika kutumia PIPOZIII.......POWER kumaliza hotuba yake

Mh. Pinda alazimika kutumia PIPOZIII.......POWER kumaliza hotuba yake

Jana hapa Mwanza, waziri mkuu alikuwa akihitimisha ziara yake mkoani Mwanza ambayo mbali na kuligarimu taifa kwa matumizi ya hela kutokana na msafara mrefu uliokuwepo, lakini umemalizika kwa fedheha kubwa kwa upande wa waziri mkuu.

Waziri alikuwa na ratiba ya kuhutubia wananchi viwanja vya Sahara, katika kuhutubia kwake, maneno yote ya chama chake hayakupokelewa na wananchi walikusanyika kumsikiliza, ilimbidi atumie maneno ya CHADEMA kumaliza hotuba yake.

CCM OYEE......watu kimya, PIPOZIII......power tena kwa shangwe kubwa.

Na ilikuwa ajbu pale Wenje alipotaka kuhutubia kwani alifikishwa jukwani kwa kubebwa.