Tuesday, May 14, 2013

MCHAKATO WA KATIBA MPYA KUZUILIWA MAHAKAMANI

MWENYEKITI WA JUKWAA LA KATIBA AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI JIJINI DAR ES SALAAM KUHUSU MAAMUZI HAYO AMBAYO WAMEYAFIKIA YA KWENDA MAHAKAMANI KUZUIA MCHAKATO WA KATIBA MPYA

MAELEZO KIDOGO

         Jukwaa la katiba Tanzania limetangaza rasmi kwenda mahakamani kusimamisha mchakato mzima wa kutapatikana kwa katiba mpya kwa kile walichokisema kuwa ni mchakato huo kwenda kinyume na makubaliano yaliyotangawa na serikali wakati mchakato huo unaanza
      

        Tamko ilo limetolewa na mwenyekiti wa jukwaa hilo bw DEUS KI KIBAMBA leo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini dar es salaam

         Bw KIBAMBA amesema wamefikia uamuzi huo baada ya juhudi zao nyingi walizozifanya ikiwemo kuonyesha mapungufu mengi yaliyojitokeza katika mchakato huo kutokufanyiwa kazi jambo ammbalo amesema ni kuwaburuza watanzania ambao wengi wanategemea kupata katiba imara

     Aidha bw KIBAMBA amesema kuwa ni lazima tume ya katiba ikubali kuwasikiliza wadau wakiwemo wanasiasa,taasisi binafsi pindi zinapoikosoa mchakato huo ili waweze kutengeneza katiba imara nay a watanzania wote
 
         Katika hatua nyingine ukwaa la katiba Tanzania limemwandika barua raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania ya maombi ya kukutana naye kwa lengo la kumweleza hali halisi ya mchakato huo wa katiba na mapungufu ambayo wao wameyaona

No comments: