Monday, May 13, 2013

REGINALD MENGI KUTOA MILIONI 1 KILA MWEZI KWA TWEET ITAYOMKUNA KILA MWEZI, HII NDO JINSI YA KUJISHINDIA

Upo kwenye Twitter? Kama haupo fanya haraka ujiunge sababu kuna ulaji huko!! Mwenyekiti mtendaji wa makampuni ya IPP, Reginald Mengi amesema kuanzia mwezi huu, atakuwa akitoa shilingi milioni 1 kwa kila tweet itakayomfurasha.
mengi2
Not too fast though…… Sio tweet zile za ‘I’m having fun being singe, #TeamSingle, tupa kuleee! Mengi anataka ulikune jicho lake kwa tweet yenye akili ambayo inaweza kuchangia kwa namna moja ama nyingine kupunguza umaskini uliokithiri nchini.
“Umaskini umekuwa sugu. Kwa mwaka1 anzia Mei ntatoa sh1m kila mwezi kwa tweet nitakayochagua kuwa bora kushinda vita na umaskini,” ametweet leo.
Ameongeza kuwa Tweet hiyo iende kwake, yaani mtu akiandika tweet afanye kummention ili aione. That’s the way to go Mr. Mengi. Kazi kwenye wazee Twira!!!

No comments: