Monday, June 10, 2013

BAADA YA KIPIGO MOROCCO STARS YAREJEA HIVI ASUBUHI HII

 Wachezaji wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager kutoka kulia Athumani Iddi 'Chuji', Amri Kiemba na Nadir Haroub 'Cannavaro' wakiwasili Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere asubuhi ya leo kutokea Morocco walipokwenda kucheza na wenyeji na kudungwa 2-1 katika mechi ya Kundi C kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Dunia mwakani nchini Brazil. Stars ilifungwa 2-1 bao lake likifungwa na Kiemba.

Wachezaji wanatoka Uwanja wa Ndege  na kuelekea kambini Tansoma Hotel, kuanza maandalizi ya mchezo ujao dhidi ya Ivory Coast wikiendi ijayo

Mbwana Samatta

Nahodha Juma Kaseja akimpa posho yake Shomary Kapombe baada ya kufika Uwanja wa Ndege Dar es Salaam. Mwingine kushoto ni Vincent Barnabas

Wanapanda basi kuelekea kambini

Kutoka kulia Mrisho Ngassa, Kapombe na Thomas Ulimwengu

Katibu wa TFF, Angetile Osiah akizungumza na Kocha Kim Poulsen 

Angetile akizungumza na Mkuu wa Msafara wa Stars nchini Morocco, Crescentius John Magori na Ofisa wa TFF, Saad Kawemba katikati

Ndondi hadi Dar; Erasto Nyoni akimtania kumpiga ngumi Ally Mustafa 'Barthez' anayejikinga kwa mifuko

No comments: