Friday, June 7, 2013

GAZETI LA MAWIO HATIHATI KUFUNGIWA


MKURUGENZI WA IDARA YA HABARI MAELEZO ASSA MWAMBENE


 Waandishi wa habari nchini wametakiwa kutambua kuwa na wao wana wajibu mkubwa  wa kulinda amani ya nchi badala ya kuandika habari ambazo zinaweza kuigawa nchi kwa misingi ya kidini,kisiasa kikabila ama kikanda

       Hayo yamesemwa na mkurugenzi wa idara ya habari maelezo bw ASSA MWAMBENE wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu gazeti moja la leo liitwalo MAWIO  lililochapisha habari ambayo kwa mujibu wa mkurugenzi huyo amesema ni habari ambayo inachochea udini serekalini

     Amesema katika gazeti hilo limeeleza kuwa viongozi wa madhehebu wa kikristo wamepitisha azimio kuwa wasitishe uhusiano wao na serikali kwa kuwa serikali inawatenga wakristo huku likiweka picha kadhaa za viongozi wa dini jambo ambalo amesema ni uchochezi mkubwa na lazima ukemewe ili nchi iendelee kuwa na amani

       Amesema lazima waandishi watambue kuwa viongozi wa dini ni watu ambao wanalea roho za watu na wanaheshimika sana na waumini wao hivyo kitendo cha kuwachafua kwenye vyombo vya habari ni kuwashushia hadhi na heshima walionayo kwa waumini wao

    Aidha katika hatua nyingine bw MWAMBENE amesema idara ya habari maelezo inamtaka mhariri wa gazeti hilo kufika mara moja katika ofisi zao ili kutoa utetezi juu ya habari hiyo kabla sheria haijachukua mkondo wake

PICHA NA MAKTABA

No comments: