Sunday, June 30, 2013

YAMETIMIA TIZAMA HELCOPTA ATAKAYO ITUMIA OBAMA LEO AKITUA BONGO

SIMU YAMPONZA MWANAFUNZI WA MSASANI SEKONDARI, APEWA KIPIGO CHA MBWA ..........






KIBAKA Rajabu Hamisi Juma (15), Mwanafunzi wa shule ya Sekondari ya Msasani, iliyoko Manispaa ya Moshi, Mkoani Kilimanjaro, amenusurika kuuwawa na wananchi wenye Hasira kali baada ya kufamaniwa mchana wa leo akiiba katika Duka la mfanyabiashara Paulo Maile.

Kibaka huyo ambaye ni mkazi wa Pasua, amekutwa na masahibu hayo baada ya kuingia dukani hapo kwa kudhani kuwa mhudumu wa duka yuko mbali na ndipo alipokutwa akiwa tayari ameshaiba Simu, aina ya Nokia huku akijaribu kuficha Laptop iliyokuwa dukani hapo.

Akizungumzia mkasa huo, kibaka Rajabu huyo aliamua kufanya hivyo kwa ajili ya kukosa ada ya kulipa shule kutokana na wazai wake kukataa kumlipia ada anayodaiwa

shuleni hapo.

Tukio hilo lililowaacha mdomo wazi baadhi ya mashuhuda waliofika dukani hapo , limetokea leo majira ya saa 6:10 mchana katika duka la Nguo lililloko katika mtaa wa double Road, barabara kuu ya Moshi-Dar es salaam linalomilikiwa na mfanyabiashara Paulo Maile mkazi wa Soweto.

Kamera ya TAIFA LETU.com ilifika katika eneo la tukio na kukuta kijana huyo akishushiwa kipondo na mhudumu wa duka hilo aliyefahamika kwa jina moja la George.Huu hapa ni mkanda mzima wa tukio lenyewe:

Amando Tarimo ambaye ni mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo akishusha kipondo kwa kijana Rajabu Hamisi aliyekutwa akijaribu kuiba katika duka la mfanyabiashara Paulo Maile, Leo Mchana.


Duka la maile lililoibiwa leo lafungwa muda mfupi baada ya jaribio hilo kuzimwa na wasamaria wema

Gari la Maile lilikiwa ilmeachwa nje ya duka hilo, Maile alilazimika kuongozana na Polisi kutoa maelezo ya mkanda mzima




Gari la Polisi likiondoka na mhalifu katika eneo la tukio


Vijana wa Boaz wakiondoka na Kibaka huyo aliyenusirika kufa mikononi mwa Raia Wema
George akitoa Maelezo kwa mashuhuda wa tukio la wizi nje ya duka hilo


George aendelea na Maelezo


Kibaka Rajabu Hamisi (Jezi ya Manchester Utd) akiomba msamaha baada ya kufumaniwa dukani katika jaribio la wizi, Paulo Maile ambaye ndiye mmiliki wa Duka (shati la mistari), George (shati jekundu katikati) na mmoja wa mashuhuda wakimsikiliza kibaka huyo dukani hapo


Rajabu akipakizwa kwenye gari la polisi leo mchana 
 
SOURCE ::KIJIJICHETU BLOGPOST

Saturday, June 29, 2013

UJIO WA OBAMA WAPINGWA NA WANANCHI WA AFRICA KUSINI.TIZAMA WALIVYOANDAMANA KUPINGA UJIO WAKE



 Waandamanaji Nchini Afrika Kusini wakiwa wamebeba mabango yanayopinga kuja Kwa Raisi Obama nchini Humo wakati wa maandamano ya Amani ya Kupinga Kuja Kwa Obama Katika Jiji la Pretoria Nchini Afrika  jana Jioni - Juni 28

 Waandamanaji Nchini Afrika Kusini Wakisali mbele ya Bango linalopinga Kuja kwa Raisi Obama Nchini Humo wakati Raisi Obama alipotua Nchini Afrika Kusini Jioni ya jana  Juni 28

 Waandamaji wa Nchini Afrika Kusini wakiwa wanasali mbele ya Ubalozi wa Marekani wakati wa maandamano ya kupinga kuja kwa Raisi Obama Nchini Humo jana  wakati Raisi Obama alipotua Nchini Humo Kwa Ziara ya Siku 2 ..

Mmoja wa waandamaji nchini Afrika Kusini ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja akiwa amebeba moja ya Bango ambalo Linamwita Raisi OBAMA kuwa ni Mpishi wa Ikulu ya Marekani kama linavyosomekana na kuendelea kuelezea kuwa sera za Marekani ni tatizo.Mwandamaji huyu alibeba bango hilo jana  Juni 28 wakati wa maandamo ya amani kuelekea mbele ya Ubalozi wa Marekani NChini humo kwa kupinga Kuja Kwa OBAMA Nchini Mwao.Picha Zote na REUTERS/AFP

Friday, June 28, 2013

CHUKUA MUDA WAKO KUTIZAMA JINSI ITALLY ILIVYONGOLEWA NA HISPANIA JANA


HISPANIA imeitoa Italia katika Kombe la Mabara kwa ushindi wa matuta wa 7-6 mjini Fortaleza, kufuatia sare ya bila kufungana ndani ya dakika 120 katika mchezo wa Nusu Fainali usiku huu.
Wataliano walifungwa na Waspanyola katika Fainali ya Euro mwaka jana wameshindwa kulipa kisasi na sasa Fainali ya michuano hiyo mwaka huu Jumapili Uwanja wa Maracana, itawakutanisha wenyeji La Roja na Brazil wenyeji.
Leonardo Bonucci wa Italia alikosa moja ya penalti 14 na Jesus Navas akaweka nyavuni mkwaju wa mwisho na kuipeleka Hispania Fainali.
Close shave: Spain moved through to the Confederations Cup final after beating Italy on penalties in Fortaleza
Ni tishio: Hispania wametinga Fainali ya Kombe la Mabara kwa kuifunga Italia kwa penalti mjini Fortaleza
Dramatic: Spain triumphed 7-6 in a dramatic shootout to set up a dream final against Brazil
Ushindi wa mbinde: Hispania wakishangilia 7-6 na sasa watamenyana na Brazil
Heartbreak: Italy were left devastated after pushing the world and European champions the distance
Maumivu: Italia wameng'oka

Si zaidi ya mwaka uliopita, Italia walipigwa 4-0 mjini Kiev, lakini The Azzurri waliwasili Fortaleza wakiamini kisasi kinawezekana, ingawa haikuwa hivyo.
Mikwaju ya penalti;  Jesus Navas alifunga a ushindi na kufanya 7-6 , baada ya Leonardo Bonucci mkwaju wake kuota mbawa.
Wengine wote waliotangulia walifunga; upande wa Hispania ni Sergio Busquets,  Juan Manuel Mata,  Sergio Ramos, Gerard Pique, Andries Iniesta na Hernandez Xavi.
Italia ni Riccardo Montolivo, Andrea Pirlo, Sebastian Giovinco, Daniele De Rossi, Alberto Aquilani na Antonio Candreva.
Kikosi cha Hispania kilikuwa: Casillas, Arbeloa, Sergio Ramos, Pique, Jordi Alba, Xavi, Busquets, Iniesta, Pedro/Mata dk79, Torres/Javi Martinez dk94 na Silva/Jesus Navas dk52.
Italia: Buffon, Maggio, Bonucci, Barzagli/Montolivo dk45,Chiellini, Candreva, De Rossi, Pirlo, Marchisio/Aquilani dk79, Giaccherini na Gilardino/Giovinco dk91.
Off target: Italy blinked first in the shout-out when Leonardo Bonucci fired over at 6-6
Anakosaaa: Leonardo Bonucci mkwaju wake uliota mbawa
Decisive: Jesus Navas stepped up to score the winning penalty and send Spain to the final
Ya ushindi: Jesus Navas alifunga ya mwisho, chini anashangilia
Jesus Navas
Jesus Navas

Glamour: Worldwide superstar Shakira was in the stands in Fortaleza
Shakira alikuwapo jukwaani Fortaleza 
This one is for you: Pique celebrates Spain's victory by the tightest of margins
Hii ni kwa ajili yako: Pique akishangilia ushindi wa Hispania
Support: Shakira was watching her partner Pique in action for Spain 
Shakira jukwaani
Greetings: Shakira meets FIFA president Sepp Blatter in the VIP lounge
Shakira alikutana na Rais wa FIFA, Sepp Blatter katika eneo la VIP uwanjani
Support: Shakira was watching her partner Pique in action for Spain
Shakira akimuangalia mpenzi wake Pique akiichezea HispaniaOn the box: A spectator enjoys the party atmosphere in Fortaleza
Shabiki
Evens: The teams were locked at 0-0 after 120 minutes in the all European semi-final
Dakika 120 ziliisha 0-0 
Outnumbered: Italy's Giorgio Chiellini tries to win a header against Sergio Ramos and Gerard Pique
Giorgio Chiellini wa Italia akijaribu kupiga kichwa katikati ya Sergio Ramos na Gerard Pique
Effort: Fernando Torres attempts a shot on goal as Gianluigi Buffon watches
Jitihada: Fernando Torres alifumua shuti lililopanguliwa Gianluigi Buffon
Stretch: Christian Maggio gets his head to the ball in front of Spanish goalkeeper Iker Casillas
Anateleza: Christian Maggio alikaribia kumtungua kipa wa Hispania, Iker Casillas
On the ball: Manchester City's David Silva attempts one of his elusive runs
David Silva akipasua
Held his nerve: midfielder Andres Iniesta slotted his penalty past Buffon in the Italian goal
Andres Iniesta alimtungua Buffon kwa penalti

BAADA YA KASEJA KUTEMWA SIMBA ARUDI KWAO KIGOMA .AONGELEA MUSTAKABALI WAKE




Siku moja baada ya klabu ya Simba kupitia mwenyekiti wa kamati ya usajili Zacharia Hans Pope kuthibitisha kwamba golikipa mkongwe wa timu hiyo Juma Kaseja hatoongezewa mkataba wa kuendelea kuitumikia klabu hiyo aliyoichezea kwa takribani miaka 10, leo hii mtandao huu umepata nafasi ya kuongea na Juma Kaseja kutaka kujua anazungumziaje uamuzi huo wa Simba.

Kaseja ambaye ni golikipa namba moja wa timu ya taifa ya Tanzania kwa sasa yupo kwao mjini Kigoma alipoenda kupumzika baada ya kumaliza majukumu yake timu ya Taifa hivi karibuni, amezungumza na mwandishi wa mtandao huu Johnson Matinde akiwa kwao Kigoma kuhusu mustakabali wake wa soka baada ya kutemwa na Simba pamoja na mambo mengine.

Juma Kaseja akijifua na vijana wadogo mkoani Kigoma wanaotaka kufuata nyayo zake.

Akizungumzia kuhusu suala la kutoongezewa mkataba mpya na Simba, Juma Kaseja alisema kwamba taarifa hizo yeye amezisikia kwenye vyombo vya habari kama watu wengine walivyosikia na hajapata taarifa rasmi: "Jana nikiwa natokea Tanga nilipokuwa nikapata taarifa za kuhusu masuala yangu na Simba. Klabu kupitia viongozi wake imeshaongea kuhusu suala hili na mie itafika siku nitaongelea kwa kina kuhusu jambo hili, ila kwa sasa ni kweli mimi sio mchezaji wa Simba na nisingependa kuzungumzia kuhusu wao."

Akizungumzia kuhusu mustakabali wake wa soka baada ya kuachana na Simba, Kaseja alisema: "Mimi ni mchezaji mpira, hii ndio kazi yangu hivyo nitaendelea kucheza mpira. Sasa kama unavyoniona nipo hapa kwetu nafanya mazoezi ili niwe bora kwenye kazi yangu. Mengine kuhusu ni timu gani nitachezea msimu ujao ningependa tuyaache kwa sasa, utakapofikia muda muafaka wa kuzungumzia then nitaongelea jambo hilo."

Kaseja akiwa mjini Kigoma amekuwa akijifua kwenye uwanja wa Shule ya msingi Kaluta, shule ambayo Juma Kaseja alisoma na uwanja wa shule hiyo ndio ambao alianzia career yake ya soka na ndio maana kila anapokwenda mapumzikoni nyumbani kwao Kigoma hupenda kufanya mazoezi uwanjani hapo na baadhi ya wachezaji chipukizi.