Monday, December 23, 2013

YAMETIMIA TENAA YANGA YAMTIMUA KOCHA WAKE ERNEST BRANDTS MUDA HUU

MUDA mfupi uliopita klabu ya soka ya Yanga imetangaza kusitisha mkataba na kocha wake Ernest Brandts baada ya kutoridhishwa na mwenendo wa timu hiyo.

Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Yanga, Baraka Kizuguto, mkataba wa Brandts ambaye ni raia wa Uholanzi umesitishwa rasmi leo hii asubuhi na ameshakabidhiwa barua ya kumtaarifu juu ya hali hiyo.

“Tumesitisha mkataba na kocha wetu na ameshakabidhiwa barua yake, huo ni uamuzi wa uongozi mzima wa Yanga, kila kitu kimeenda sawa katika kuachana naye,” alisema Kizuguto.

Tetesi za Brandts kutimuliwa zilizagaa jijini Dar es Salaam tangu jana muda mfupi baada ya Mwenyekiti wa Yanga, Yussuf Manji kwamba hata kama klabu itaamua kuachana na kocha huyo itafuata taratibu zote.

Uamuzi huo wa Yanga unaonekana pia kuchagizwa zaidi na kipigo cha mabao 3-1 dhidi ya Simba katika mchezo maalum wa kirafiki maarufu kama Nani Mtani Jembe uliochezwa wikiendi iliyopita Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

WABUNGE WAANZISHA MKAKATI MPYA WA KUMNG'OA WAZIRI MKUU MIZENGO KAYANDA PINDA KISA UTENDAJI MBOVU WA KIONGOZI HUYO KATIKA SERIKALI YA RAIS JK.

BAADHI ya wabunge wameanzisha mkakati wa kumwondoa madarakani, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda katika kile wanachodai kuwa hawaridhishwi na utendaji wake serikalini.
Hiyo ni dalili kwamba kung’oka kwa mawaziri wanne kutokana na matokeo ya ripoti ya utekelezaji wa Operesheni Tokomeza Ujangili hakujamnusuru Pinda, kwani baadhi ya wabunge wanaendelea na msimamo kwamba naye ajiuzulu kwa kushindwa kuwasimamia wenzake.

Mawaziri waliong’oka baada ya Rais Jakaya Kikwete kutengua uteuzi wao kutokana na ripoti iliyowasilishwa na Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira ni Mawaziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Shamsi Vuai Nahodha, wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi, Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Dk Mathayo David Mathayo na Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki.

Hatua hiyo ya Rais Kikwete inatafsiriwa na wengi kama njia ya kuwapoza wabunge na kumwokoa Pinda ambaye ikiwa atang’oka itamaanisha kuundwa upya kwa Baraza la Mawaziri.
Habari ambazo zimelifikia gazeti hili jana zinasema wabunge 26 wametia saini fomu maalumu ya kutaka Bunge litumie mamlaka yake ya kikatiba kumng’oa Pinda kwa kumpigia kura ya kutokuwa na imani naye.
 
Kwa mujibu wa Ibara ya 53 A(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977, Bunge linaweza kupitisha azimio la kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu, endapo itatolewa hoja kupendekeza hivyo.

Kwa mujibu wa Ibara hiyo, hoja ya kumpigia kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu inapaswa kuungwa mkono na wabunge wasiopungua asilimia 20 ya wabunge wote.

Mbunge wa Kasulu Mjini (NCCR-Mageuzi), Moses Machali alisema hili jana kuwa ukusanyaji saini za wabunge aliouanzisha Ijumaa jioni unakwenda vizuri.

“Kung’oka kwa mawaziri wale wanne inatosha kuthibitisha kuwa Pinda amepoteza uhalali wa kuwa Waziri Mkuu kutokana na kushindwa kuwasimamia walio chini yake,” alisema Machali.

“Rais tunaweza kumuacha, lakini Pinda ndiye mtendaji mkuu wa shughuli za Serikali. Kama wapo mawaziri wameboronga ni wazi na yeye anaingia moja kwa moja katika hilo kapu,” alisema na kuongeza:

“Kama kweli tunataka taifa lisonge mbele kutoka hapa tulipo ni lazima tumuondoe Pinda…….. amekuwa mpole mno, mzito kufanya uamuzi na analea matatizo.”

Hata hivyo, alisema wabunge waliosaini fomu hiyo, wote wanatoka kambi ya upinzani na kusema wabunge wengi wa CCM aliowafuata kuwaomba watie saini wanaogopa au wanasita kufanya hivyo. MWANANCHI

HAYA NDIO MAPOKEZI YA ZITO KABWE KIGOMA,NI ZAIDI YA MFALME


SOMA MAGAZETI YOTE YA LEO HAPA JUMATATU



.
.
.
.
.
.
.
endelea nayo hapa--------

Wednesday, December 18, 2013

BREAKING NEWZZ:MV MAGOGONI YANUSURIKA AJALI

Kivuko kikubwa cha Mv Magogoni kinachofanya safari zake kati ya Kivukoni na Kigamboni jijini Dar es Salaam kimekosa muelekeo majini katika bahari ya Hindi kikiwa na abiria na magari baada ya injini zake kushindwa kufanya kazi,Mpaka sasa sababu ya injini kushindwa kufanya kazi hazijatoka.
Shuhuda anasema ‘Tulikua wanatoka Dar kwenda Kigamboni,hatua chache kabla ya kufika Kigamboni injini zilizima,baada ya kuzima zikaja Tag kwa ajili ya kutuvuta mpaka ng’ambo ya pili ambayo ni Kigamboni,na ilituchukua dakika 45 mpaka kuvutwa ng’ambo ya Kigamboni’
Taarifa kamili zinafata endelea kufatilia kupitiaHABARI24 BLOG


ALIYEBAKWA NA KAPUYA ATINGA MAREKANI,KIMEWAKA BUNGENI.HAYO NA MENGINE YASOME HAPA KUTOKA KWENYE MAGAZETI JUMATANO DESEMBA 18/ 2013


.
.
.
.
.
.
.
.
ENDELEA NAYO CHINI------------

HIKI NDICHO KIINGILIO RASMI CHA MECHI YA MTANI JEMBE JUMAMOSI


IMG_8659
Kiingilio cha chini kwenye mechi ya Mtani Jembe kati ya Simba na Yanga itakayochezwa Jumamosi (Desemba 21 mwaka huu) ni sh. 5,000. Kiingilio hicho ni kwa viti vya rangi ya kijani ambavyo ni 19,648.
Kwa upande wa viti vya rangi ya bluu kiingilio ni sh. 7,000, viti vya rangi ya chungwa itakuwa sh. 10,000, VIP C kiingilio ni sh. 15,000, VIP B itakuwa sh. 20,000 wakati VIP A yenye viti 748 tu tiketi moja itapatikana kwa sh. 40,000. 
Tiketi zitaanza kuuzwa siku moja katika vituo mbalimbali, mchezo huo utafanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10 kamili jioni.
Vituo ambavyo tiketi hizo zitauzwa keshokutwa (Ijumaa) ni Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Sokoni Kariakoo, mgahawa wa Steers ulioko mtaa wa Ohio/Samora, Oilcom Ubungo, Kituo cha Mafuta Buguruni, Dar Live Mbagala, Uwanja wa Uhuru, na BMM Salon iliyoko Sinza Madukani.
Mechi hiyo itachezeshwa na Ramadhan Ibada (Kibo) kutoka Zanzibar, ambapo atasaidiwa na Ferdinand Chacha wa Bukoba, na Simon Charles kutoka Dodoma. Mwamuzi wa akiba ni Israel Nkongo wa Dar es Salaam wakati mtathimini wa waamuzi ni Soud Abdi wa Arusha.

JANGA LINGINE CHADEMA,WARAKA MWINGINE WA SIRI WASAMBAZWA TENA,SASA UNAMUHUSU MBOWE,WAAINISHA UFISADI WAKE MWANZO MWISHO,USOME HAPA WOTE,ALIYEUANDIKA NI HABIBU MCHANGE

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgO_Y990zEgeiBST_JoqN7wsKR8p9ou0ngZ8bnAcjSXeFCkSU9-DYha8CD5lpLbs5akSLdqbOujHNi2VycXimDnqtDBvlK9aHdyQLaB2YSlYVSPp6ePHNZ_CRSwxWwlx0CecmDxBvdogsVc/s1600/Mbowe.jpg 
Imeandikwa na 
Habibu Mchange
0762178678:
-------
 Juzi niliandika kuhusu unafiki wa MBOWE kuwahadaa Watanzania ya kwamba yeye hanunuliki, nilitoa ushuhuda wa MBOWE kupokea million 100 kutoka kwa ROSTAM AZIZ aliyekuwa mwanamkakati muhimu wa ushindi wa Urais kwa mgombea wa CCM mwaka 2005 Mheshimiwa JAKAYA KIKWETE, ambapo pesa hizo zilipokelewa mwezi oktoba 2005 na kumfikia mbowe kupitia kwa mke wake ndugu LILIAN MTEI MBOWE, na kumfikia MBOWE ambaye kipindi hicho alikuwa anagombea URAIS kupitia CHADEMA,

hapa mbowe sio tu kwamba alinunuliwa, alihongwa ama kutumiwa kuwadhoofisha wapinzani waliokuwa na nguvu kipindi hicho, bali pia alidhihirisha namna gani yeye ni mpinzani mtiifu kwa CCM (alikubali kutumika) na ni MNAFIKI ALIYETUKUKA.

Leo tarehe 18.12.2013, Magazeti kadhaa yameripoti juu ya muendelezo wa unafiki wa MBOWE na vibaraka wake.

Magazeti yameandika pamoja na mambo mengine, kwa ufupi kabisa hivi ifuatavyo.
ENDELEA KUUSOMA HAPA-----------

BREAKING NEWS:WATU 200 WALIOKUWA WAKISAFIRI KWA NDEGE YA ETHIOPIAN AIRLINE WANUSURIKA KUFA BAADA YA KUTUA DHARURA KWENYE UWANJA WA NDEGE WA ARUSHA




Taswira ya picha eneo la tukio
             Habari iliyoifikia hivi punde toka jijini Arusha, inaeleza kuwa Ndege ya abiria aina ya Boeing 787 ya shirika la ndege la Ethiopia (Ethiopian Airlines) mchana huu imeshindwa kutua kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) kutoka na hitilafu iliyokuwepo Uwanjani hapo na kulazimika kutua kwa dharula kwenye Uwanja wa Mdogo wa Arusha,hali iliyopelekea Ndege hiyo kusimama nje kabisa ya uwanja huo huku abiria zaidi ya 200 wakiwa ndani ya ndege hiyo mpaka sasa bila ya kushuka.
 
Wataalam wa Ndege wapo eneo la tukio hivi sasa kutafakari namna watakavyoweza kuwashusha abiria hao na kutafuta namna ya kuweka sawa mambo ili Ndege hiyo iweze kuruka.
 
Globu ya Jamii inaendelea kufatilia kwa ukaribu tukio hilo,na tutaendelea kufahamishana kadri taarifa itakavyokuwa ikitufikia.  PICHA NA MDAU WETU KUTOKA ARUSHA
CHANZO: BLOG YA PAPARAZI

PICHA YA BASI MOJA LILILOLETWA KWA AJILI YA MAJARIBIO YA BARABARA YA MABASI YAENDAYO KASI.


Tuesday, December 17, 2013

TAARIFA MUHIMU KUTOKA TIGO,YAWATANGAZIA NEEMA WATEJA WAKE

Na Karoli Vinsent

     KAMPUNI ya Simu za mkononi Nchini ya Tigo  imewatangazia Neema wateja wake baada ya kuzindua promosheni kabambe iitwayo “Cheza kwa Furaha Unaposhinda kitita”itakayowawezesha watumiaji wa huduma ya Tigo pesa kujishindia zawadi mbalimbali za fedha taslim  zenye jumla ya shilling bilioni moja.  

      Akizungumza na waandishi wa habari leo,Meneja Mawasiliano wa Tigo Bw.John Wanyacha amesema kwamba promesheni hii mpya inatokana na kampuni  hiyo kuweka kipaumbele kuwapa wateja wake sababu ya kutabasamu na fursa ya kuweza kubadilisha maisha yao  kupitia huduma za kutuma na kupokea pesa.

      “Jumla ya shilingi milioni 150 itashindaniwa.Kutakuwa na zawadi na fedha taslim milioni10 kila mwezi kwa wateja 10 kila mmoja,fedha taslim shiling milioni mbili kila wiki kwa wateja 20 kila mmoja na fedha taslimu shilingi laki mbili  kwa wateja   50 kila mmoja”alisema Wanyancha
ENDELEA HAPO CHINI--------

KUELEKEA MWISHO WA MWAKA KAMANDA MPINGA ATOA ONYO KWA MADEREVA

KAMANDA WA POLISI KIKOSI CHA USALAMA BARABARANI DCP MOHAMED MPINGA AKIZUNGUMZA NA WANAHABARI MAPEMA LEO JIJINI DAR ES SALAAM.AMBAPOAMEWATAKA MADEREVA WA MABASI YAENDAYO MIKOANI NA WALE WA HAPA DAR ES SALAAM KUWA MAKINI KUHAKIKISHA WANATII SHERIA ZA USALAMA BARA BARANI KATIKA KIPINDI HIKI CHA MWISHO WA MWAKA ILI KUEPUKA AJALI ZA MARA KWA AMARA AMBAZO HUWA ZINATOKEA KIPIONDI KAMA HIKI,AKIZUNGUMZA NA WANAHABARI AMESEMA KUWA NI LAZIMA MADEREVA WAHAKIKISHE MAMBO YAFUATAYO YANAFWATWA IKIWEMO KUTOJAZA ABIRIA KUZIDI KIPIMO,KWA SAFARI NDEFU KUWEPO KWA MADEREVA WAWILI,MAGARI KUTOSAFIRI ZAIDI YA SAA SITA USIKU,KUHAKIKISHA MAGARI YANA MIKANDA,PAMOJA NA MAMBO MENGINE AMBAYO NI KINYUME NA SHERIA ZA USALAMA BARABARANI.
WANAHABARI WAKISIKILIZA KWA MAKINI

TANZANIA NA KANADA ZASAINI MKATABA WA USHIRIKIANO MUDA HUU KATIKA OFISI ZA WIZARA YA UCHUKUZI

BALOZI WA KANADA NCHINI TANZANIA ALEXENDER LEVEQUE ALKISAIN MKATABA WA MAKUBALIANO YA USHIRIKIANO BAINA YA NCHI YAKE NA TANZANIA MUDA HUU KATIKA OFISI ZA WIZARA YA UCHUKUZI JIJUINI DAR ES SALAAM
            Wizara ya uchukuzi tanzania na shirika la biashara la nchini kanada leo wameseini mkataba wa makubaliano ya ushirikiano baina ya nchi hizo mbili katika secta mbalimbali kubwa zaidi ikiwa ni katika maswla ya reli na biashara. akizungumzana wananahabari jijini dar es salaam baada kusaini makubaliano hayo katibu mkuu wa wizara ya uchukuzi bi  MONICA MWAMUNYANGE amesema kuwa tanzania imekuwa na ushirikiani wa muda mrefu na nchi ya kanada katika maswala ya reli hivyo mkataba huo ni kwa ajili ya kukuza na kuendeleza makubaliano hayo ya siku nyingi.
TUNAKABIDHIANA--KATIBU MKUU WA WIZARA YA UCHUKUZI TANZANIA BI MONICA MWAMUNYANGE AKIKABIDHIANA NABALOZI WA KANADA NCHINI MIKATABA WALIYOSAINI MUDA MFUPI ULIOPITA

Monday, December 16, 2013

AZAM TV YAANZA RASMI KUHUDUMIA WATEJA WAKE LEO,TIZAMA HABARI NA PICHA

JB AU BONGE LA BWANA ALIKUWEPO
MKURUGENZI MKUU BW RHYS TORINGTON AKISALIMIANA NA WASANII WA BONGO MUVIES KATIKA MAKAO MAKUU YA AZAM LEO ASUBUHI


             AzamTV leo imeanza kutoa huduma zake rasmi katika makao makuu yaliyopo barabara ya Nyerere, jijini Dar es Salaam.



             Huduma za matangazo ya AzamTV zilianza kupatikana hewani Kuanzia Ijumaa Desemba 6, 2013 kwa kuwawezesha wateja waliounganishwa kwenya kisimbuzi kungalia bure hadi hii leo ambapo huduma kwa malipo inaanza rasmi kwa ada ya shilingi 12,500 kwa mwezi.



         Kwa kuanzia huduma ya AzamTV itahusisha chaneli 50 zinazojumuisha chaneli maarufu za kimataifa, chaneli maarufu za ndani na chaneli tatu maalumu za Azam ambazo ni:



·         Azam One – burudani kwa familia kutoka Afrika, sehemu kubwa ya matangazo itakuwa kwa lugha ya Kiswahili.

·         Azam Two – vipindi maalum kutoka sehemu mbalimbali za dunia 

·         SinemaZetu – Chaneli maalumu kwa tamthilia za kitanzania kwa saa 24.



          Kwa pamoja, chaneli tajwa zitawapa wateja wigo mpana wa kufaidi matangazo bora ya michezo, tamthilia, watoto na maisha.



         Ofisi ilifunguliwa rasmi na Bw. Yusuf Bakhresa: Mkurugenzi Mtendaji wa Azam Media Ltd.



          “Ofisi hii ya makao makuu ambayo kwa hakika ni ya kuvutia ni kielelezo cha nia thabiti ya Azam Media kufanya kazi kwa umakini katika shughuli ya utangazaji hapa Tanzania. Dira yetu ni kutoa burudani ya kiwango cha juu kwa familia kwa bei nafuu kote nchini, na baadaye kote barani Afrika. Hili ni jambo ambalo kila mmoja hapa nchini anapaswa kujivunia.” Alisema Bakhresa



          Rhys Torrington: Afisa Mtendaji Mkuu wa Azam Media Ltd alisema: “Naona faraja kubwa kwamba leo hii AzamTV  ipo sokoni kwa ajili ya kila mtanzania. Tutahabarisha, kuelimisha na zaidi ya yote tutaburudusha watu kote nchini. Huduma yetu inapatikana kwa watu wote – situ katika ofisi hizi lakini pia kupitia mtandao wetu unaohusisha zaidi ya mawakala 50 katika kila mkoa. AzamTV ni ya kudumu”



          Azam Media pia inawekeza katika utayarishaji wa vipindi vipya kupitia kampuni yake tanzu, Uhai Productions, kwa kushirikiana na watayarishaji wa vipindi wa hapa Tanzania.



YUSUFU AKIWA NA BAADHI YA WASANII WA BONGO MUVIE AMBAO NAO WALIKUWA MIONGONI MWA WALIOSHUGHUDIA TUKIO HILO

Displaying DSC03820.JPG
Displaying DSC03819.JPG
MKURUGENZI MTENDAJI WA AZAM TV BWANA YUSUFU BAKHRESA AKIKATA UTEPE KUASHIRIA KUANZA RASMI KWA HUDUMA ZA AZAM TV

CLABU YA SIMBA HAKUKALIKI, MASHABIKI WAJIANDAA KUVAMIA KLABU YA YANGA, WATAKA KULIPA KWENDA KUMNYOFOA EMMANUELI OKWI, WADAI AMEWASALITIU

UMATI MKUBWA WA MASHABIKI WA KLABU YA SIMBA WAKIWA KATIKA JENGO LA KLABU YAO WAKIJIANDAA KWENDA KATIKA KLABU YA YANGA KWENDA KUMCHUKUA MCHEZAJI WAO WA ZAMANI ALIYESAJIRIWA NA YANGA KATIKA DIRISHA DOGO, bW eMMANUEL OKWI. MASHABIKI HAO WANATAKA WAELEZWE SABABU ZA KUUZWA MCHEZAJI HUYO WAKATI WAO BADO HAWAJAPATA FEDHA ZAO  WALIZOMUUZA MCHHEZAJI HUYO HUKO TUNISIA.

HAPA WAKIWA WANAJADILIANA BILA KUPATA MAJIBU YA UHAKIKA, HATA HIVYO MASHABIKI HAO WAMEISHIA KUPIGA DOMO HUKU MCHEZAJI HUYO AKITAMBULISHA LEO HII KATIKA KLABU YA YANGA

HAPA WAKIMTAZAMA MWANDISHI MWANDAMIZI WA FULLHABARI WAKATI AKIWAHOJI WASHABIKI HAO NI KWANINI WAPO HAPO NA SULUHISHO LAO NI NINI HASA.MASHABIKI WAMESEMA HAWALI MPAKA KIELEWEKE NA KWAMBA RAGE ATAWAJUA WAO KAMA NI MASHABIKI AMA WANACHAMA WANAOTAMBULIKA KISHERIA, WAMESMA KUWU UZEMBE WA MWENYEKITI UMEWAFANYA WAKOSE YOTE KUANZIA MCHEZAJI JUMA KASEJA NA WA SASA BW. EMMANUEL OKWII,

HAPA WAKIFAFANUA KWA HISIA, WANACHAMA HAO WAMESEMA RAGE HAIFANYII FAIR KLABU YAO NA NDIO MAANA WACHEZAJI WOTE MUHIMU WANAONDOKA KUELEKEA KLABU PINZANI

ULIKUWA MSHIKESHIKE WA AINA YAKE BAADA YA WALE WANAOJIITA KUW AWANACHAMA WENYE HASIRA KALI KUVAMIA JENGO LA KLABU HIYO NA KUPIGA KAMBI YA MUDA AWAKITAKA MWENYEKITI WAO NA WAO WENYEWE WAANDAMANE WAENDE KLABU YA YANGA KUUMCHUKUA MCHEZJI WAO, MPAKA TUNAKWENDA MITAMBONI WANACHAMA HAO HAWAJAONYESHA DALILI ZAKWENDA KLABU YA YANGA KUDAI MCHEZAJI WAO

HUYU NDIO OKWI AKISAINI YANGA MIAKA MIWILI


KLABU ya Yanga SC ya Dar es Salaam imemsajili mshambuliaji wa zamani wa Simba SC, Emmanuel Arnold Okwi raia wa Uganda kwa Mkataba wa mia miwili na nusu. 
Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya klabu ya Yanga, Abdallah Ahmed Bin Kleb amesema jioni hii mjini Dar es Salaam kwamba wamemsajili Okwi na ataanza kuichezea timu hiyo mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Bara na michuano ya Afrika.

exclusive---RATIBA YA MAKUNDI UEFA HII HAPA


exclusive---HIVI NDIVYO MABINA WA CCM MWANZA ALIVYOUWAWA NA WANANCHI JANA





                Aliyekuwa mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza MABINA ameuwawa na wananchi wenye hasira kali kwa kupigwa mawe huko maeneo ya Kiseke jijini Mwanza.Chanzo cha kuuwawa ni kwamba mabina aliwanyang'anya ardhi wananchi hao na kesi ikawa mahakamani na leo mchana Mabina bila kibali cha mahakama alikuwa anapanda miti na kujenga msingi wa nyumba ndipo wananchi wakaenda kumhoji iweje anapanda miti na kuweka msingi kwenye viwanja hivyo ilhali kesi ipo







Saturday, December 14, 2013

SAKATA LA KUFUNGIWA MWANAHALISI LAIBUKA BUNGENI,NAIBU WAZIRI MAKALA AMPINGA RAIS JK WAZI WAZI


Na Karoli Vinsent

  NAIBU Waziri wa Habari na Michezo Amosi Makala amepingana hadharani  Rais Jakaya kikwete kuhusu sakata la kulifungia Gazeti la mwanahalisi.

      Hayo yaligundulika wiki hii katika vikao vya bunge vinavyoendelea mkoani Dodoma katika kipindi cha maswali na majibu,ambapo mbunge wa Mbinga Mashariki kapteini John Komba(CCM) alipokuwa anauliza swali kuhusu utaratibu  uliotumiwa na serikali katika kuyafungia magazeti ya mtanzania pamoja  mwanahalisi.

  “kwanini Serikali ilitumia nguvu katika kuyafungia magazeti ya Mwanahalisi pamoja na Mtanzania wakati tayari serikali ilikuwa imeshawaonya  wahariri hao na hao wahariri wa magazeti hayo wakakubali kosa na kuomba Radhi”aliuliza Komba
ENDELEA HAPO--------

WAANDISHI WA HABARI ZAIDI YA 200 WAHITIMU LEO TSJ,FAIDI PICHA HIZO






MKUU WA CHUO NAYE ALIPEWA ZAWADI

 ENDELEA NA PICHA HAPO CHINI------

EXCLUSIVE----CCM YAWAJIA JUU MAWAZIRI MIZIGO,NAPE ATOA TAMKO KALI KWA JK LEO,ATAKA WAFUKUZWE MARA MOJA,AWATAJA KWA MAJINA


PICHA NA MAKTABA
NA KAROL VICENT ------ CHAMA cha Mapinduzi (CCM) kimemtaka Rais Jakaya kikwete kuwatimua malamoja moja  mawaziri mizigo kwa kushindwa kuwatumikia wananchi na Kuendesha Siasa za umangi meza.


      Hayo yalisemwa na Katibu  wa itikadi na uwenezi Nape Nnauye wakati akizungumza na wahariri wa vyombo vya habari, makao makuu ya chama hicho jijini Dar es salaam,Nape alisema kamati kuu ya chama cha mapinduzi ya CCM imefikia maamuzi ya kumtaka Rais Kikwete kuwafukuza kazi mawaziri hao kutokana na kutowatumikia wananchi na kuendesha Siasa za Umangi meza  katika wizara zao.
ENDELEA KUSOMA HAPO CHINI--------

Friday, December 13, 2013

EXCLUSIVE---WANAWAKE WAWILI WAKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA ZAIDI YA KETE 200 ZIKIWA TUMBONI,NI UWANJA WA NDEGE WA JK NYERERE,WALIKUWA WANAPELEKA CHINA

KAMANDA WA UWANJA WA NDEGE WA JK NYERERE ASP RENATUS CHALYA AKIZUNGUMZA NA WANAHABARI LEO OFISINI KWAKE.

Na karoli Vinsent

        MIEZI michache kupita  Tangu waziri wa uchukuzi dokta Harisoni Mwakyembe kufanya mabadiliko kwenye uwanja wa kimataifa wa Uwanja wa ndege wa Mwalimu JK NYERERE ,watu wa wawili wamekamatwa wakisafirisha madawa ya kuleva.
 ENDELEA HAPO CHINI--------

Thursday, December 12, 2013

AJALI MBAYA MKOANI TANGA: BASI LA BURUDANI LAPATA AJALI MBAYA LIKITOKEA KOROGWE KUELEKEA JIJINI DAR,WATU ZAIDI YA 12 WAHOFIWA KUFARIKI NA MAJERUHI ZAIDI YA 50. PICHA ZA TUKIO HIZI HAPA









Basi la Burudani baada ya ajali leo Wilaya ya Handeni, Tanga.
Basi la Burudani leo limepata ajali kijiji cha Taula Wilaya ya Handeni, Imeripotiwa mpaka sasa watu zaidi ya 12 wamefariki na majeruhi zaidi ya 55. Watu 4 wamepelekwa MOI na KCMC. Tuwaombee majeruhi.
Hospitali ya wilaya ya Korogwe.
Majeruhi wakipatiwa matibabu.
Mkuu wa Wilaya ya Korogwe, Mrisho Gambo ( kushoto) akiangalia mmoja wa majeruhi akipatiwa matibabu.
Manesi wakiendelea na matibabu kwa majeruhi.
Mmoja wa majeruhi akiwa amelazwa kwenye benchi.
Wananchi wakiwa eneo la Hospitali.
PICHA ZOTE KWA HISANI YA MKUU WA WILAYA YA KOROGWE, MRISHO GAMBO.