Tuesday, January 21, 2014

CHADEMA SASA YAJA NA MPYA,CHATISHIA KUTOSHIRIKI UCHAGUZI UJAO NCHINI,WATAWANYIKA NCHI NZIMA KUFANYA MIKUTANO,SOMA KISA KIZIMA HAPA



MWENYEKITI WA CHADEMA FREMAN MBOWE AKIZUNGUMZA NA WANAHABARI LEO.PICHA NA EXAUD MTEI
Na Karoli Vinsent

        CHAMA cha democrasia na maendeleo nchini “Chadema’ kimetishia kutoshiriki Uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2015 kama endapo Tume ya Uchaguzi nchini haitofanya marekebisho kwenye Daftari la kudumu la wapiga kura.ENDELEA HAPO--------



         Hayo,yalisemwa leo na mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe wakati akizungumza na Waandishi wa Habari makao Makuu ya Chama hicho jijini Dar es Salaam,ambapo alisema Chama hicho kimeamua kufanya maamuzi hayo kutokana na Tume hiyo kuwanyima Fursa vijana katika chaguzi mbalimbali hapa nchini.

       “Tunaiambia Tume ya uchaguzi Nchini endapo hawatalifanyia Marekebisho Daftari hili sisi hatutashiriki uchaguzi mkuu mwakani ili kuonyesha chadema tunauchungu juu ya vijana ambao wanakosa fursa ya kupiga kura kwani chadema tulifanya sensa tukabaini vijana Milioni tano wanakosa nafasi ya kupiga kura kutokana na kutofanyiwa marekebisho Daftari hili”alisema mbowe
        
         Mbowe ambaye ni Kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni na pia ni Mbunge wa jimbo la Hai kwa tiketi ya Chama hicho alisema kitendo cha tume hiyo kusema haina fedha huko ni kuwadanganya Wananchi

      “Sheria inasema wazi kabla ya uchaguzi kufika lazima Daftari hilo lifanyiwe marekebisho ili kuwapa nafasi vijana waliofikisha umri wa kupiga kura waweze kushiriki au hata wale waliopoteza kwa bahati mbaya kadi zao za kupigia kura waweze kusaidiwa lakini leo tume hiyo inasema haina fedha,Chadema tunasema huu ni ubabaishaji”alisema Mbowe

       Katika hatua nyingine Chama hicho kimenzindua Ziara ya nchi nzima kwa lengo la kukijenga chama hicho.
“Chadema tumeanza ziara ya Nchi nzima ili tuwafikia wananchi popote walipo ili kuwapa ujumbe pamoja na kuwashirikisha na kuwapa nafasi katika kujadiri matatizo yanayowakuta huko walipo kwenye sehemu zao za kuishi”alizidi kufafanua Mbowe
            
     Ziara hiyo itachukua wiki tatu ambapo chama hicho kimesema kitatumia usafiri wa Ndege pamoja na usafiri wa Bahari pamoja na nchi kavu kwa lengo la kuwafikia Wanachi popote walipo.
      
 Kuhusu Katiba mpya

       Kuhusu katiba mpya Mwenyekiti huyo wa Chadema ilikitadhaharisha Chama cha Mapinduzi CCM pamoja na wabunge wake kuwa chadema hawatokubali kutumia katiba ya zamani kwenye uchaguzi ujao

     “Nasema chadema hatutakubali kurudishwa nyuma kwenye katiba ya Zamani eti kwa hoja ya Wabunge wachache wa CCM pamoja na mwenyekiti wao,kwa maslai yao binafsi na sisi Chadema tunasema hatutokubali kurudi nyuma na ili tutumie katiba ya zamani” alisema Mbowe
 
    Mbowe,alisema Maelezo ya Jaji Walioba yanaonyesha jinsi gani wananchi wanataka katiba mpya.  

No comments: