Wednesday, January 8, 2014

WIZARA YA MALIASILI KWAWAKA MOTO TENA,WATUMISHI 21 WASIMAMISHWA LEO NI HUJUMA ZA UJANGILI,NYALANDO ATANGAZA HALI HATARI

Wizara ya maliasili na utalii tanzania kupitia idara ya wanyama pori tanzania imewasimamisha kazi watumishi wake 21 kwa makosa mbalimbali yakiwemo ya hujuma juu ya wizara hiyo

akizungumza na wanahabari leo jijini dar es salaam naibu waziri wa wizara hiy mh LAZARO NYALANDO amesema kuwa katika watumishi waliosimamishwa 11 wanatoka kikosi dhidi ya ujangili  arusha,4 pori la akiba rukwa,1 kutoka pori la akiba seluu,3 pori la akiba maswa,na 1 kutoka pori la akiba lukwika-lumesule-msanjeshi.

amesema kuwa makosa makubwa yaliiyofanywa na watu hao kuw ni vitendo vya rushwa katika mapori hayo pamoja na kuwasaidia majangili katika kufanya uhalifu wao huo,ambapo ameeleza kusikitishwa sana na vitendo hivyo

Aidha jana jeshi la polisi kwa kushirikiana na wizara ya maliasili na utalii lilimkamata askari wa wanyama pori mmoja bw AGOSTINO LORI mkoani singida akiwa na bunduki mbili na ndege aina ya heroe au flamingo 12 uani mwa nyumba yake kinyume na sheria .

Naibu waziri amesema kuwa mtu huyo miongoni mwa maaskari wa wanyamapori ambao wanashiriki katika vitendo vya hujuma,rushwa,na ujangili dhidi ya wanyama porihuku akiwa ameaminiwa na nchi yake kama askari wa wanyama pori.amesema kuwa kitendo hiko kinatia aibu sana nchi na hatua kali dhidi yake zitachukuliwa mara moja

No comments: