Sunday, January 5, 2014

YAMETIMIA CHADEMA,KITILA MKUMBO NA MWIGAMBA WAVULIWA UANACHAMA,DK SLAA ASEMA YA ZITO YANAKUJA



Dk.Kitila Mkumbo aliyetimuliwa uanachama Chadema.

       KAMATI Kuu ya Chadema iliyokutana Januari 3-4, 2014 katika Ukumbi wa Mbezi Garden, jijini Dar es Salaam imeamua kuwavua uanachama Dk. Kitila Mkumbo na Samson Mwigamba kuanzia jana.Maamuzi hayo ni baada ya kunasa mawasiliano mbalimbali ya Zitto Kabwe na washirika wake akiwemo anayejulikana kwa jina la Chadema Mpya.

       Akizungumza na wanahabari leo, Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Willbroad Slaa amesema malengo ya waraka wa mabadiliko waliokutwa nao wahusika hayakuwa ya kisiasa tu bali yalikuwa na lengo la kuimaliza chadema na kuwabomoa viongozi wa chama.
 
      Ameongeza kuwa, chama kinawatangazia wanachama wote na wapenzi wote kutokushiriki mikutano ama shughuli zozote za kisiasa zitakazoandaliwa na Zitto Kabwe na washirika wake kwa jina la Chadema.
Samson Mwigamba ambaye naye amevuliwa uanachama wa Chadema.

No comments: