MKURUGENZI WA KITUO HIKO DEUS KIBAMBA AKIZUNGUMZA NA WANAHABARI |
Na Karoli Vinsent
KAULI
aliyopata kuitoa Waziri Mkuu Mizengo Pinda bungeni kuwataka polisi wawapige
wapinzani, na kauli ya juzi ya Rais Jakaya Kikwete kuwaagiza wafuasi wa Chama
Cha Mapinduzi (CCM), wajibu mapigo pale wanaposhambuliwa na wapinzani, imeelezwa
kuliingiza taifa vitani,
Nacho
Kituo Cha taarifa kwa Wananchi (TCIB)kimeanza mawasiliano na Mwendesha Mastaka
Mkuu wa Mahakama ya Kimataifa ya uharifu dhidi ya Binadamu(ICC) Bi Fatou
Bensouda kumwomba atume timu ya wataalamu wake kuja Tanzania kufanyia
Uchunguzi na Tathmini kuhusu kauli hizo iliwaweze kuifungulia mashtaka Serikali
ya Tanzania.
Hayo,yasemwa
Leo,jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Kituo hicho, Deus Kibamba wakati wa
Mkutano na Waandishi wa Habari ambapo alisema wameamua kufanya Maamuzi hayo kwa
kuona Amani ya nchi inaanza kutoweka kutokana na viongozi kutoa matamshi
yanayochochoe uvunjifu wa amani.
ENDELEA HAPA----------
“Tumeamua
kuchukua hatua hii kufanya mawasiliano na Mwendesha Mastaka Mkuu wa Mahakama ya
Kimataifa ya uharifu dhidi ya Binadamu(ICC) Bi Fatou Bensouda baada ya kuwa na
hofu kuwa tukiachi matamshi”
“ haya
yaendelee,kunaweza kutokea fujo kubwa na kupelekea mauaji ya ajabu huko
tunapoelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2015,leo kiongozi mkubwa kama Rais anatoa
kauli hizi tena mbaya,hivi anafikiria wakati anatoa kauli hizi,leo anafikiri
amani hii ikivunjika yeye nani atabaki hapa”alisema Kibamba
Kibamba ambaye
ni Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba Nchini alisema Taifa la Tanzania litaingia
kwenye machafuko kwani nchi ya Jirani ya Kenya dalili zake zilikuwa kama za
Tanzania.
“Mimi kwenye
uchaguzi wa Kenya wa Mwaka 2007 nilikuwepo na Dalili za machafuko zilitokana na
viongozi kama hawa kutoa kauli za kukashifu na katoa amasa kwa wananchi
kulipiza kisasi,leo hawo greengurd wakishambulia redgurd au redgurd wakiwashambulia
Greengurd kunamtu atapona,manaake amani ya nchi ndio inavunjika hapo”alisema
Kibamba.
Ikumbukwe tamko
la Kibamba limekuja kutokana na kauli ya Rais kikwete, wakati Akifungua
mkutano wa NEC ya CCM juzi mjini Dodoma, Rais Kikwete aliwataka wanachama wa
chama hicho kuacha unyonge kwani uvumilivu waliokuwa nao umefika kikomo chake.
Alisema chama
hicho kinaingia kwenye uchaguzi mdogo katika Jimbo la Kalenga mkoani Iringa,
kinashindana na vyama vingine ambavyo alisema ni wagomvi, maana kwao ugomvi
ndiyo sehemu ya mwongozo wa kufanya kazi ya siasa.
“Tulizungumza
nalo hilo kwenye Kamati Kuu, tulikubaliana kuacha unyonge. Ndiyo, kwenye Kamati
Kuu tumekubaliana, tumesema jamani watu wote waende wakaseme tumekubaliana
kuacha unyonge,” alisema huku akicheka na kupigiwa makofi na wajumbe wa NEC.
Rais Kikwete
ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu, alitolea mfano wa tukio lilitokea Kahama mkoani
Shinyanga, ambapo kijana mmoja alitolewa macho kwa bisibisi, na tukio la Igunga
ambapo kijana mmoja alimwagiwa tindikali katika uchaguzi mdogo wa jimbo hilo.
“Acheni unyonge
na hata katika taarifa ya habari leo (jana) mtoe hivyo hivyo. Na muache habari
zote mseme hii tu (waandishi wa habari). Uvumilivu una ukomo wake,” alisema
huku wajumbe wakiendelea kumpigia makofi.
“Nalisema kwa
sababu yanayotokea yanasikitisha sana. Pale Igunga kijana yule wamemmwagia
tindikali, pale Kahama kijana ametolewa macho kwa bisibisi,” alisema.
Uchaguzi mdogo
wa ubunge Jimbo la Kalenga lililopo mkoani Iringa unatarajiwa kufanyika Machi
16, mwaka huu, huku tayari vyama vya CCM na CHADEMA vikiwa vimetaja wagombea
wao.
Katika
hatua nyingine kituo hicho cha kuwasemea wananchi kimezengumzia uchaguzi mdogo
wa madiwani kata 27 na kusema uchaguzi huo ulikuwa na kasoro nyingi sana
ikiwemo idadi ndogo ya wapiga kura pamoja vitendo vya utekaji pamoja na utesaji
walivyokuwa wanafanyiwa wagombe na wapiga kura.
No comments:
Post a Comment