Monday, February 17, 2014

TIGO YAHITIMISHA PROMOTION YAKE LEO KWA KISHINDO-DEREVA BAJAJI ANYAKUA MILION KUMI MCHANA HUU

BW FADHIL SULEMAN AKISHANGILIA KWA FURAHA BAADA YA KUKABIDHIWA MFANO WA HUNDI YA SHILINGIM  MILLION KUMI KAMA MSHINDI WA TIGO
        Kampuni ya simu za mikononi yaTIGO TANZANIA leo imehitimisha promotion yake ya CHEZA KWA FURAHA UNAPOSHINDA KITITA kwa kuwakabidhi washindi wake wa mwisho ambapo kivutio kikubwa ni dereva bajaji aliyejishindia shilingi million kumi
         
 Akizungumza na wanahabari leo jijini dar es salaam mratibu wa promotion hiyo MERY RUTTA amewataja washindi wa zawadi za mwisho leo kuwa ni MWANTUM JUMA aliyeshinda million mbili ambaye ni mama ntilie,na mshindi wa million kumi ambaye ni dereva bajaji maeneo ya kijitonyama bw FADHIL SULEMAN.
   
       Akizungumza baada ya kupata zawadi hiyo bw FADHIL amesema kuwa hakuamini hata kidogo baada ya kupigiwa simu kuwa ameshinda lakini sasa anaanza kuamini kuwa ameshinda kweli na kusema kuwa itamsaidia kwenye mambo yake ya kila siku.
          
         Leo ndio imefikia mwisho wa promotion hiyo ambayo meneja mwasiliano wa tigo bw JOHN WANYANCHA amesema kuwa lengo la shindani hilo ilitokana na kampuni hiyo kuwapa kipaumbele wateja wake kwa kuwapa puia sababu ya kutabasamu na fursa ya kuweza kubadilisha maisha yao.katika kipindi cha miezi miwili jumla ya billion 1.2 zimenyakuliwa na wateja wa tigo katika promotion hiyo

MRATIBU WA PROMOTION HIYO MARY RUTTA AKIMKABIDHI HUNDI

No comments: