Thursday, February 13, 2014

TPDC LAVIVAA VYOMO VYA HABARI NCHINI.SOMA HAPA



        NA KAROL VICENT
        
         SHIRIKA  la maendeleo ya Petrori Nchini ( TPDC) Limekanusha Taarifa zilizotolewa na vyombo mbalimbali vya Habari, juu  ya utafiti wa Mafuta na Gesi asilia unaoendelea katika maeneo ya Kilosa_kilombero,Tanga na Maeneo ya Kilimanjaro kuwa mafuta yamegundulika.
SOMA HAPA----------------

         
         Hayo,yalisemwa leo Jijini Dar Es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji shirika hilo wakati wa Mkutano na Waandishi wa Habari, Yona Killagane   alisema taarifa hizo sio za kweli kuhusu Upatikanaji wa Gesi.
       
       “Tunapenda kuwafahamisha wananchi kuwa Taarifa hizo sio Sahihi ,tunaomba wananchi  wajue kuwa ili kuwa na uhakika kuwa eneo Fulani ilnamafuta au gesi ni lazima kuchimba kisima/visima  vya utafiti katika eneo,maeneo husika na kuona kuwa gesi  au mafuta vyakitoka yenyewe kisima au visima hivyo”
    
           “Mpaka sasa hakuna hata kisima kimoja kilichochimbwa katika maeneo tajwa hapo juu bali kilichofanyika mpaka sasa ni utafiti wa awali uliohusisha uchukuaji wa takwimu za mitetemo na kufanyia uchambuzi”alisema Killagane
          
     Vilevile,Killagane alisema utafiti huo umebaini maeneo  hayo  yana kina  (Thickness) cha kutosha cha Miamba tabaka ambayo utafiti wa mafuta na gesi unaweza kufanyika .

        
        Katika, hatua nyingine Mkurugenzi huyo akasema Mamlaka iliyopewa uwezo wa kutoa taarifa za ugunduzi wa rasilimali za mafuta na gesi asilia ziko chini ya  waziri wa Nishati na Madini na wala sio chombo kingine chochote ,

No comments: