Friday, February 14, 2014

UJANGILI TANZANIA----MBUNGE SHELUKINDO AMJIBU MSIGWA ,ASEMA ANAUDANGANYA UMMA



Na Karoli Vinsent
                SIKU chache kupita Baada ya Mbunge wa Iringa Mjini Peter Msigwa kumshutumu Rais Jakaya Kikwete kuwa serikali yake imeshindwa kuzuia ujangili hapa nchini, MBUNGE wa Kilindi (CCM), Beatrice Shelukindo Amemvaa mbunge msigwa nakusema anadanganya Umma.
         
         Pia,Shelukindo amesema Serikali ya Jakaya Kikwete imefanya kazi kubwa ya kupambana na ujangili unaoendelea hapa nchini,
Hayo,yamesemwa Leo na Mbunge huyo jijini Dar Es Salaam,Wakati wa Mkutano na waandishi wa Habari ndipo mbunge huyo alisema Anashanga Kauli aliyoitoa Mbunge Msigwa juu ya Rais kikwete kuhusu Ujangili unaofanyika hapa nchini.
ENDELEA HAPA---------------



         “Leo Mbunge msigwa anamshambulia Rais kuwa Serikali ya CCM ndio inayofanya Ujangili,nataka niwambie wananchi kauli ya mbunge msigwa sio ya kweli kwani serikali ya Rais kikwete imefanya kazi kubwa sana ya kupambana na vitendo vichafu vya ujangili”
          
          “Leo ukiangali sensa kuhusu kufa kwa tembo imepungua kutokana na kazi kubwa inayofanywa na Serikali ya Rais kikwete leo utasemaje Serikali ya kikwete haifanyi jitihada za kutokomeza Vitendo vya ujangili”alisema Shelukindo
          
           Hayo,yalitokana Habari iliyoandikwa kwenye Gazeti la Dailmail la Nchini uingereza toleo la tarehe 6 mwezi huu, ambalo liliishutumu Serikali ya CCM kuwa  inahusika na vitendo vya ujangili vinavyoenderea hapa nchini na kukishutumu chama hicho kinapata pesa kutokana na vitendo vya ujangili na kukiendereza Chama hicho,

           Mwandishi wa Gazeti hilo pia likamshutumu Rais kikwete kuwa anashindwa kuwachukulia hatua vinara wa vitendo vya ujangili,kwasababu ni marafiki zake,baada ya kauli hiyo ndipo Waziri wa Maliasili na utalii akakanusha taarifa hiyo na kusema sio za kweli.
        
             Ndipo,mbunge wa Iringa mjini Piter msigwa CHADEMA  akaibuka na kusema Makala iliyoandikwa na Gazeti hilo la  kuwa kuwachulia hatua  makada ya wa chama cha mapinduzi ambao wanahusika na vitendo vya ujangili hapa nchini.
         
         Ikumbukwe,Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa, alimtuhumu Katibu Mkuu wa CCM kuwa ni mmoja wa watuhumiwa kwa ujangili na kwamba serikali haimchukulii hatua, hivyo kuwaasa Watanzania wamweke mbali na tembo.

         Alisema afadhali apige kelele ili tembo wasichukuliwe, twiga wasisafirishwe, apige kelele watu wapate maji, kuliko kukaa kimya aonekane ana nidhamu twiga na tembo wauawe au wasafirishwa

No comments: