Tuesday, July 22, 2014

CHAMA CHA WALIMU TANZANIA WATISHIA KUGOMA TENA,SOMA SABABU HAPA

Na Karoli Vinsent

        CHAMA cha Walimu nchini (CWT) kimesema kitapinga kwa nguvu zake au kuitisha mgomo wa walimu nchi nzima,endapo kama serikali itapitisha sheria ya mpya ya Kupunguza mafao ya wastaafu wanachama wa Mifuko ya pesheni ya watumishi (PSPF) na watumishi wanachama wa LAPF.  


        Tishio hilo limetolewa Leo Jijini Dar es Salaam,na Rais wa Chama cha Walimu (CWT) Gratian Mukoba wakati wa Mkutano na Waandishi wa Habari,ambapo alisema chama hicho baada ya kupata pendekezo kutoka Wizara ya Kazi na Ajira kwa kushirikiana na Mamlaka ya mifuko ya Jamii (SSA) khusu punguzo hilo kwa watumishi wa umma ikwemo walimu.

          Ambapo chama cha walimu katika kikao chake cha kamati ya utendaji ya Taifa(KUT)  kilichokaa mjini Morogoro walijadili pendekezo hilo na kuja maamuzi ya kupinga kwa nguvu zote mpango huo ambao unalenga kuwadhulumu walimu pamoja wafanyakazi wengine mafao ya kustaafu kama utapitishwa kutungiwa sheria.
Mukoba,alizidi kusema mpango huo ukipitishwa na kuwa sheria utapunguza kinua mgongo cha walimu na watumishi wengine wa umma.

       “Hatuwezi kukubali mpango huu,kwani utazidi kumfanya mwalimu awe masikini zaidi,mpango huu utamaliza kiiunua mgongo cha walimu,kwani zaidi ya nusu kile wanachokipata kwa sheria iliyopo sasa,wakati wanajua watumishi hawa wanaishi katika hali ya umasikini wa kutisha”alisema Mukoba.

         Mukoba ambaye kitaaluma ni Mwalimu,aliyataja maeneo hayo ambayo watayapinga kwa nguvu zote ikiwemo
Kupunguza  malipo ya Pesheni ya mkupuo yanayolipwa na mifuko ya PSPF na LAPF kutoka asilimia 50 ya sasa hadi asilimia 33.3 ya mshahara wa  mwezi wa Mtumishi kabla ya kustaafu,
Vilevile alizidi ya kuyataja maeneo mengine  ni kupunguza makadirio ya Umri wa kuishi kwa mwanachama baada ya kustaafu toka miaka 15.5 baada ya kustaafu hadi miaka 12.5,

          Katika hatua nyingine chama hicho cha walimu kimesema wamegundua sababu ya Serikali kufanya Rafu hiyo mbaya kwa Watumishi wa umma ni kutokana na Serikali kudaiwa pesa nyingi sana.
“Tumechunguza tumegundua sababu ya Serikali kuendelea kuwakandamiza watumishi hawa wa Umma ni kutokana na serikali zaidi ya Trilioni 7,”

        “Kwa pamoja tunaiomba sana serikali isitishe mpango huu wanaotaka kuleta,na kama wanatafuta njia nyingine kuiokoa mifuko hii,basi watafute njia nyingene”alisema Mukoba  



No comments: