Monday, July 14, 2014

EXCLUSIVE--BAADA YA JANUARY MAKAMBA KUTANGAZA NIA URAIS,MOTO WAWAKA,LOWASA SASA HALI NGUMU--SOMA KISA HIKI

Na Karoli  Vinsent

           KILE kinacho tafsiliwa kwamba wapambe wa waziri mkuu wa zamani Edward Lowassa wameanza kumgeuka na kuanza kujiondoa katika harati zake za kuchukua usukani wa Juu wa uongozi wa nchi kwenye uchaguzi mkuu mwakani 2015 ndani ya CCM,zimeanza kuonekana Mtandao huu umebaini.

           Mtandao huu umedokezwa kwamba aliyekuwa mpambe wa kiongozi huyo Edward Lowassa,ambaye ni  aliyekuwa Katibu Mkuu mstaafu wa Chama cha Mapinduzi CCM,Yusuf Makamba tayari amejitoa kwenye kundi la kumpigania Waziri mkuu huyo aliyejiuzuru.

        Kwa mujibu wa vyanzo vya kuaminika ambazo mwandishi wa Mtandao,amezipata zinasema awali Mzee Makamba alikuwepo katika upande ambao ulijitosa kuhakikisha Lowassa anachukua Urais katika uchaguzi mkuu mwakani 2015,lakini sasa ameamua kujiondoa.


         Chanzo hicho makini kinasema sababu ya Katibu huyo wa Mstaafu wa CCM,kujiondoa ni Kutokana na Mwanae January Makamba,ambaye tayari ametangaza nia y a kuwania nafasi hiyo  Urais na tayari baadhi ya watu wameanza kumuunga mkono kutokana na uamuzi wake wa kujitosa katika nafasi hiyo.

          January makamba ambaye ni Naibu waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia,alitangaza uamuzi huo wiki iliyopita wakati akifanyia mahojiano na Shirika la Utangazaji la BBC,aliitaja nia yake kugombania nafasi hiyo ya Amiri Jeshi mkuu,na kusema sasa ni wakati wa Vijana kushika nafasi hiyo.

         Mtoa taarifa huyo aliuambia mtandao huu kwamba Mzee Makamba tayari  amejitoa katika upande wa Lowassa na  ameacha pigo kwenye harakati hizo.

         “Sikufichi hizo taarifa ni za kweli mpambe mwenzetu  tuliyekuwa naye wakati tukipigania mzee wetu huyo lowassa kuingia ikulu,eti naye amejitoa na kuanza kumsapoti mwanae Janury makamba,ambaye naye ameanza kukubalika kiasi chake kwa watu mbalimbali ikwemo wachambuzi wa kisiasa”

       “Na hili nakuhakishia ni pigo kubwa sana kwa Mzee wangu Lowassa kwasababu nafasi aliyekuwa anaifanya ni kubwa sana katika harakati hizo ndugu”alisema mtoa taarifa huyo.

        Naye Mjumbe Halmashauri kuu ya chama cha Mapinduzi CCM NEC,kutoka mikoa ya Kanda za juu kusini aliyezungumza na Mwandishi wa Mtandao huu  kuhusu hali hiyo,kwa sharti la kutoandikwa Jina mtandaoni alisema lowassa anawakati mgumu sana katika harakati zake kwani tayari  nguvu yake kwa kundi lake inaanza kumeguka.

          “Mzee yusufu Makamba tayari  amejiondoa sasa katika upande wa kundi la lowassa .sasa utagemea nani anaushawishi katika kundi la lowassa,kwa hili tusitegemee jipya kwenye Nafasi yake,hebu ona jinsi anavyopigwa vita na kila Kada wa CCM,”alisema Mjumbe huyo.

        Kwa upande wake Msomi wa Masula ya Kisiasa kutoka chuo Kikuu Dodoma,Seiph Yahaya alisema waziri mkuu aliyejiuzuru Edward Lowassa anawakati mgumu sana kuingia Ikulu kwani kila msaka urais anayeibuka anampinga yeye ,na kwa mtazamo huu  chama cha CCM,uwenda kikapasuka vibaya wakati wa kumteua mtu anatakayeshika nafasi ya urais kwenye uchaguzi mkuu mwakani 2015.


No comments: