Na Karoli
Vinsent
HUJUMA zinazodaiwa kufanywa na
viongozi wa chama cha mapinduzi CCM kwenye mchakato wa upatikanaji wa Katiba
Mpya na kupelekea Wajumbe wanaounda umoja wa Katiba ya Wananchi
UKAWA kususia vikao vya Bunge la Katiba ,sasa hali hiyo imeanza kuwa chungu kwa viongozi hao Mtandao umebaini.
Vyanzo vya Uhakika kutoka
ndani ya chama cha Mapinduzi CCM, zinasema chama hicho kinafikilia kuukubali
muundo wa Serikali tatu ambao unatokana na Rasimu ya maoni ya wananchi,kuachana
na Rasimu ya kipropaganda ya chama hicho inayozungumzia muundo wa Serikili
mbili.
Chama hicho kikongwe kulichopo kusini
mwa jangwa la Sahara ambacho kipo madarakani,kimeamua kulegeza kamba na kufuata
maoni ya wananchi kutokana na kupata shinikizo kubwa kutoka kwenye Madhehebu ya
Dini nchini pamoja msimamo mkali uliowekwa na Muungano wa Kutetea Katiba ya
Wananchi,UKAWA.
Licha ya Rais Jakaya
Kikwete,kutumia kila njia ili wajumbe kutoka UKAWA,kurudi kwenye bunge la
Katiba,kwenye vikao vyake vinavyotarajiwa kuendelea tena mwezi ujao,kugonga
mwamba baada ya kumtumia msajili wa vyama vya kisiasa nchini Jaji Francis
Mutungi,ambaye ameonekana kushindwa kazi hiyo ya kuwashawishi warudi kwenye
bunge hilo lilokuwa likibeza maoni wananchi.
Kwa mujibu wa mjumbe wa kamati kuu ya CC
kutoka CCM,anasema”kwa hali iliyopo kwa sasa hakuna jinsi lazima tukubali
muundo wa serikali tatu ambao umetokana na maoni ya wananchi,kwani tumemshauri
mwenyekiti wetu Rais Kikwete, akubaliane na hawa wajumbe wa UKAWA,kwani serikali
tatu ndio kila kitu”alisema mjumbe huyo
wa juu kamati ya chama cha mapinduzi ya ccm.
Mwandishi wa mtandao huu amedokezwa,Rais Jakaya Kikwete tayari ameipiga
chini kauli yake aliyoitoa wakati wa ufunguzi wa Vikao vya Bunge la
Katiba,ambayo alitoa maelekezo kwa wajumbe wa Bunge hilo wakubaliane na muundo
wa Serikali tatu na kupiga chini maoni ya Wananchi.
Ambapo Rais Jakaya Kikwete tayari amekutana Faragha na wajumbe wanaunda Umoja wa
katiba ya Wananchi UKAWA,ikulu jijini Dar Es Salaam ili kupata mwafaka juu ya
kukwamua mchakato wa katiba ambao aliuvuruga mwenyewe.
Chanzo hicho kilisema Mkutano kati ya
Rais kikwete na Mjumbe mwandamizi wa UKAWA,mkutano huo ulifanyika usiku wa wiki
iliyopita kutokana na ombi la Rais .wito wa Rais Kikwete kwa UKAWA ulifanyika
kwa njia ya Simu.
Kuhaha huku kwa Rais Kikwete kuukwamua
mchakato huu kumekuja baada siku mbili tangu Halmashauri kuu ya 48
bya jumuiya ya kikristo Tanzania (CCT)iliyokutana tarehe 2 na 3 mwaka huu
,kuelekeza waumini wake kupigania kuwepo serikali tatu ambayo
inapingwa vikali na CCM,
Duru za Kisiasa zinasema
mwenye uwezo wa kukwamua mchakato huu wa katiba ni Rais Jakaya Kikwete ambaye
ndio aliuharibu mwenyewe,licha ya Jitihada alizofanya mwenyekiti wa Bunge la
katiba, waziri Sitta kutumia nguvu zake zote kuwasihi wajumbe hao wa UKAWA
wanaotetea maoni ya Wananchi kurudi Bungeni.
Teyali wajumbe hao wa
UKAWA wakiwa wametoa sharti moja tu ili wajumbe hao waweze kurudi kwenye vikao
vya bunge la katiba ni kwa Wajumbe wa chama cha Mapinduzi CCM,kuacha kujadili
Rasimu ya kwao badala yake wajadili Rasimu iliyotokana na Maoni ya
wananchi.ambacho sharti hilo limekuwa ngumu sana kwa chama hicho kubaliana na
hali hiyo.
Duru hizo zilisema kama Rais
Jakaya Kikwete akishindwa kukwamua mchakato huu wa Katiba basi atakuwa amejiharibia
katika Nyanja mbalimbali za Siasa nchini,endapo akiondoka madarakani mwakani
mwezi wa kumi,na kujijengea sifa mbaya ya kiongozi aliyepelekea nchi kupoteza
mabilioni ya fedha kwenye mchakato wa katiba ambao aliuharibu mwenyewe kwa
kauli zake.
No comments:
Post a Comment