Friday, July 18, 2014

HABARI ILIYOTIKISA JIJI LEO--CHADEMA WATISHIA KUSUSIA UCHAGUZI WA MWAKANI,SOMA SABABU HAPA


Na Verynice shoo

Rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania  Mheshimiwa Jakaya mrisho kikwete  ametakiwa kuachana na itikadi za chama chake tawala ccm  katika mchakato huu wa katiba ili aweze kuinusuru taifa  na wananchi ambao hawapati haki katika katiba ya zamani

Mchakato huo ambao uliingiwa na dosari wakati wa  majadiliano yaliyokuwa yanafanyika na wajumbe wa bunge maalum la katiba baada ya kutokuelewana katika rasimu iliyokuwa mezani kwa majadiliano na kuupelekea umoja wa katiba ya wananchi ukawa kuamua kutoka nje ya bunge hilo

Rai hiyo imetolewa na mwenyekiti wa chama cha demokrasia na maendeleo chadema Mh. Freeman Mbowe wakati akizungumza na waandishi wa habari katika kikao cha ndani cha kamati kuu ya chama hicho kilichofanyika mbezi garden leo hii
Kikao hicho kitafanyika ndani ya siku mbili chenye ajenda za majadiliano ya tathmini ya muendelezo hali ya kisiasa hapa nchin,jinsi ya kuukomboa mchakato wa katiba kwa sasa taarifa za bunge maalum la katiba na bunge labajeti,maandalizi ya uchaguzi wa serikali za mitaa,utendaji wa chama na taarifa mbalimbali  na maadhimio yake


Hata hivyo aliweka wazi msimamo wa ukawa kuwa hawatakuwa tayari kurudi katika bunge la katiba kwa kushinuikizwa na watu binafsi au taasisi  binafsi bali wako tayari kurudi kwa maridhiano ya maongezi na makubaliano ya ufuatliaji wa agenda na kanuni za bunge maalumu la katiba na kujadili vilivyomo katika rasimu n asiyo vinavyotolewa na uongozi wa ccm


Rais wetu kashindwa kuingilia kati tatizo hili la bunge maalum la katiba na amewaachia watu na taasisi binafsi kutoa matamko juu ya bunge hilo sisi tutarudi kwa makubaliano na maridhiano ya ufuatiliaji wa kanuni za bunge hilo alisema kiongozi huyo



Halikadhalika kiongozi huyo alibainisha kutokuwa tayari kwa chama chake kushiriki katika uchaguzi mwaka 2015 kwa kutumia katiba ile ya zamani kwani imekuwa na makosa mengi sana na haiwezi kutumika katika uchaguzi mkuu ujao


Kwa kweli kwa upande wa chama changu sitakuwa tayari kuona mchakato huu wa katiba unapotezwa na raisi wetu na kushindwa kupatikana katiba mpya itakayo tumika kwa wananchi hata hivyo sitaipa nafasi chama changu kushiriki katika uchaguzi kwa kutumia katiba ya zamani\alisema kiongozi huyo


Vivyo hiyo amemtaka rais wa awamu hii kuachana na mambo ya kiunafiki kwa kuwadanganya wananchi juu upatikanaji wa katiba kwa kutumia chama chake hivyo aitumie nafasi hii kwa kuimarisha upatikanaji huo ili aweze kumaliza uongozi wake kwa usalama zaidi

No comments: