Saturday, July 19, 2014

LEO NDIO LEO-WATANZANIA TUUNGANE

kapombe-may7-2013(2)
KIUNGO na beki wa timu ya Taifa ya Tanzania, Shomary Kapombe amewaomba watanzania kujitokeza kwa wingi kuishangilia timu yao dhidi ya Msumbiji `Black Mambas`  katika mechi muhimu ya kuwania kupangwa hatua ya makundi ya kusaka tiketi ya kucheza fainali za mataifa ya Afrika, AFCON, mwakani nchini Morocco.
Mchezaji huyo kiraka alisema wachezaji 11 wanaocheza uwanjani hawatoshi kupata ushindi, hivyo mashabiki kama wachezaji wa 12 wanatakiwa kujitokeza kwa wingi kuishangilia Taifa Stars.
“Napenda kuwaambia watanzania wote kuwa huu ni mchezo muhimu, nawaomba watanzania waje kuisapoti timu”. Alisema Kapombe.

No comments: