Thursday, July 17, 2014

TAARIFA YA NDEGE NYINGINE YA MALAYSIA ILIYOANGUKA LEO IKIWA NA ABIRIA 295



Ndege ya Malaysia, Boeing 777 iliyokuwa inatoka Amsterdam kwenda Kula Lumpur imeanguka Mashariki mwa Ukraine karibu kabisa na mpaka wa Russia, leo, July 18.
Kwa mujibu wa CNN, waziri wa Malaysia anaehusika na mauala ya Usafirishaji amesema kuwa abiria 280 na wafanyakazi 15 waliokuwa kwenye ndege hiyo wamepoteza maisha.
Tweet ya Malaysia Airlines imeeleza kuwa ndege hiyo ilipoteza mawasiliano baada ya kutoka Amsterdam.
Kumekuwa na taarifa za awali kuwa ndege hiyo ilipigwa na na Ukraine, taarifa ambazo zimekanushwa na raisi wa Ukraine.
Rais wa Malaysia ameeleza kupitia twitter jinsi alivyosikitishwa na tukio hilo na kudai kuwa wataanza uchunguzi wa tukio hilo haraka iwezekanavyo kufahamu chanzo.
Tukio hili linatokea wakati ambapo bado ndege ya nchi hiyo, Flight 370 iliyopotea March 8 Mwaka huu bado haijapatikana.

No comments: