Tuesday, August 19, 2014

exclusive--CHAMA KIPYA CHA ACT CHAFANYA USAJILI MWINGINE ,HAWA NDIO VIONGOZI WA KISIASA WALIOJIUNGA NAO LEO


Fred Kisena,ambaye alikuwa Mkurugenzi wa Mahusiano ya Jamii na sera Taifa ya chama cha SAU  kahamia ACT akikabidhiwa rasmi kadi ya act

    Na Karoli Vinsent

        BAADA ya kuzoa wanachama wengi kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA,Chama kipya cha Siasa nchini cha Alliance for change and Transparency ACT,sasa kimezidi kuzoa wanachama wengine ikiwemo viongozi kutoka vyama vingine vya upinzani .
       
        Hayo yamejidhililisha  leo Jijini Dar es Salaam wakati walipokuwa wakitambulishwa wanachama wapya waliohamia chama cha ACT-Tanzania Mbele ya Waandishi wa habari,Ambapo Katibu Mwenezi wa Chama cha ACT-Tanzania Masega Muhamedi Masega alithibitisha kupokea wanachama wapya watatu ambao walikuwa viongozi waandamizi kutoka Chama cha Upinzani cha Sauti ya Umma SAU,
          
          Viongozi hao Waandamizi ni Fred Kisena,ambaye alikuwa Mkurugenzi wa Mahusiano ya Jamii na sera Taifa ya chama cha SAU ,Majinus Mwembe  Mkurugenzi Mkuu wa Fedha pamoja na Zabroni Shilumbi ambaye alikuwa Naibu katibu mkuu wa Sera wa chama hicho.
           
         Wakizungumza wote kwa pamoja viongozi hao wa chama cha SAU ,waliohamia chama cha ACT-Tanzania  walisema wameamia kwenye chama hicho baada ya kupendezewa sera ya chama hicho na kusema kwa sasa wanaimani chama cha ACT-Tanzania ndio mkombozi Watanzania kutoka kwenye hali ngumu ya Maisha inayowakabili.
         
          Naye Katibu Mwenezi wa Chama cha ACT-Tanzania Masega Muhamedi Masega aliwashukuru sana viongozi hao wa chama cha SAU kwa kuungana nao katika kutetea Watanzania na kusema chama hicho kitahakikisha kinashirikiana na wanachama hao kuhakikisha wanamkomboa mtanzania wa leo na kuwataka watanzania kujiunga na chama hicho kwani ndio kimbilio lao,
         
            Katika Hatua nyingine Chama hicho kipya cha Siasa cha ACT-Tanzania,kuanzia kesho kitaanza Ziara kwenye mikoa 15 kwa lengo ya kueneza na kukijenga chama hicho hadi ngazi za chini.
         
        Akizungumzia Ziara hiyo Katibu Msaidizi wa Chama hicho Leopald Luca Mohona alisema wameandaa makundi matatu yatakayogawanywa mikoa 15 ambapo kundi la kwanza litaongozwa na Mwenyekiti wa Mda chama hicho Lukas Kadawa Limbu akisaidiwa na Mjumbe wa Halmashauri kuu ya Athumani Balozi.
Ambapo ziara hiyo itatumia siku 17 kufikia majimbo 22 kwenye mikoa mitano.
Huyo anayezungumza ndio Katibu Mwenezi wa Chama cha ACT-Tanzania Masega Muhamedi Masega
      
         Vilevile Kundi Jingine litaongozwa na Makamu mwenyekiti akisaidiwa na Naibu katibu mkuu Taifa pamoja na kundi jingine pia litakalo ongozwa na Katibu Mkuu wa chama hicho Samsoni Mwigamba atakayeambatana na Katibu Uenezi wa chama hicho kwenye mikoa mengine,

No comments: