Monday, August 18, 2014

KAULI YA WEREMA SASA YALIGAWA TAIFA,LHRC NAO WAIBUKA NA TAMKO NZITO LA KUMPINGA,SOMA HAPA

Na Karoli Vinsent

   KAULI aliyoisema Mwanasheria Mkuu wa Serikali  Jaji Fredrick Werema kwamba Rais Jakaya Kikwete hana Mamlaka ya kulivunja Bunge la Katiba kwa madai ya kutokuwepo na kipengele cha sheria kitakachompa Nafasi hiyo,sasa kauli yake imezidi kupingwa kila kona.Mtandao huu unaripoti.
   
           Kauli hiyo ya Ukakasi kutoka Kwa Mwanasheria huyo wa serikali imepingwa leo Jijini Dar Es Salaam,na Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu LHRC, Harodia Sungusia wakati mkutano na Waandishi wa Habari aliuitishwa mahususi kuzungumzi uzinduzi wa Filamu yenye kulenga kuwapa elimu watanzania kuhusu mambo ya katiba mpya.

        
          Sungusia alitumia mkutano huo kutoa masikitiko yake kwa Mwanasheria Mkuu  na kusema anatoa kauli zenye kuonekana ziko kisiasa na kuacha kuzungumzia Udhaifu wake wakushindwa kupeleke kipengere kinachompa Rais Mamlaka la kulivunja Bunge Maalum La Katiba.
            
          “Nashangaa sana kwa kauli hiii ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali anavyosema Rais hana Mamlaka ya kulivunja Bunge la Katiba wakati ukiangalia Kifungu cha 25 cha sheria kinampa Rais nguvu ya kuteua na kufukuza mtu yeyote ambaye hana sifa,kama rais ananguvu wewe unasema Rais hana Mamlaka y a kulivunja Bunge la katiba hizo tunaweza kusema ni kauli za Kisiasa.alisema Sungusia
                 
             Sungusia alizidi kusema Sheria ya Mabadiliko ya Katiba mpya inanuksi kutokana na kuwepo kwa Vipengel

e vinavyosema endapo itashindikana kupatikana na kwa Katiba Basi turudi kutumia katiba ya sasa amb apo alisema hiyo ndio Nuksi.
    
                Katika hatua nyingine Kituo  hicho cha Sheria na Haki za Binadamu LHRC kwa mara ya kwanza  Kimezindua  FiLamu mpya ambayo itatumika katika kutoa elimu kwa Watazania kuhusu katiba mpya,
              
          FiLamu hiyo ambayo imeigizwa na Wasanii kutoka Tanzania wakiwemo Jengua,Masele,Mrisho mpoto pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa  Kituo hicho DKT Helen kijo Bisimba.
           
       Ambapo Filamu hiyo itazinduliwa Rasmi kesho katika Ukumbi wa Senima iliyoko karibu na Chuo kikuu cha Mlimani na Wananchi wameomba kufika bila kukosa kuja kujionea uzinduzi huo.

No comments: