Tuesday, August 19, 2014

UJIO WA REAL MADRID TANZANIA WAHISIWA KUWA CHANZO CHA KITENGE KUHAMA RADIO ONE,SOMA MKASA HUU

Na Karoli Vinsent

         SABABU za Mtangazaji Maalufu wa Kipindi cha Michezo na Burudani Maulidi Kitenge  kuipiga Chini Redio one  na Kuamia Redio mpya E.fm 93.7 ya hapa Dar Es Salaam, sasa sababu zaanza kufichuka,Mtandao huu Umedokezwa Sababu hiyo.
         
          Maulidi Kitenge ambaye ametanga rasmi mwanzoni mwa wiki hii kupitia mtandao wake  wakijamii wa facebook kwamba Miaka 14 aliyokaa redio na Kituo cha Tv cha Itv inatosha yeye kukaa mjengoni hapo na tena yeye kushindwa kuweka wazi sababu ya kuondoka hapo na kuondokea kwenye kituo kipya cha Redio cha E.fm 93.7 Dar Es Salaam,
          
     Taarifa za kuaminika Ambazo Mtandao huu umedokezwa kutoka kwenye Vyanzo mbalimbali vilivyopo hapo E.FM Redio pamoja na  Radio one zinasema sababu iliyomfanya aondoke hapo ndio sababu ambayo inahisiwa ndio itakayowafanya Watangazaji wengi waondoke Redio one.
            
      Akielezea Sababu hiyo,Mfanyakazi wa kituo redio cha Efm, alichohaamia Kitenge ambaye hakutaka Jina lake litajwe Mtandaoni alisema  mtangazaji huyo amekosa uhuru ndio ikapelekea kutoelewana na mabosi zake.
         
       “Da ni kweli Kitenge sahivi ni mfanyakazi Mwenzetu na tayari  kasaini Mkataba,ila sababu iliyomfanya aondoke pale Redio one,inatoka na y eye kuhusika katika kutengeneza Tangazo  linalohusu Ujio wa Timu ya Wazee wa Realmadrid ambao watakuja Tanzania wiki ijayo,sasa baada ya kutengeneza Tangazo lile Viongozi Radio one wakakasilika kwa yeye kutengeneza Tangazo linalohusu redio nyingine tena kwenye Studio tofauti na hapo”alisema mpashaji huyo
             
            Chanzo hicho kilizidi kusema mara baada ya kitenge kutengeneza Tangazo hilo aliitwa kujitetea na Mabosi  wa Redio one,lakini yeye alionekana kama anakosa Uhuru kutokana na kuingiliwa hata sehemu zengine ambazo hazihususiani na kazi yake kutokana na kufanya kazi pale inapohitajika,ndipo akachukua maamuzi ya kuachana Redio hiyo.
      
           Mwandishi wa Mtandao huu alimtafuta Mkurugenzi wa Redio One Deogratus Rweyunga na kutaka kujua ukweli wa taarifa hizi,ambapo Rweyunga alimtaka Mwandishi wa Mtandao huu amtafute Kitenge mwenyewe na kuzidi kusema yeye hana ugomvi na kitenge.
       
            “Hebu sikiliza Mtafute Kitenge mwenyewe,maana yeye kwenda kwenye Redio hiyo ni changamoto zengine na tunamtakia maisha mema na sisi hatuna ugomvi na kitenge kaamua kuacha kazi hapa ni sawa yeye ameona ni sahihi,na halafu unaposema Tangazo hilo alilotengeneza ndio imetufanya tukasirike na tumfukuze kazi sio kweli kwani mbona yeye katengeneza matangazo mengi ikiwemoa Tamasha la matumaini atujakasirika na limepigwa Redio nyingi sana na hatujamfukuza iweje leo ”alisema Rweyunga
           
         Mwandishi wa Mtandao huu alipomtafuta kitenge kujua ukweli wa Taarifa hizo hakuweza kupatikana mara moja kutokana na kutopatikana kwenye simu,
      

        Sababu hiyo ya kitenge Kuondoa Redio one  iliwai kutolewa mara kwa mara kwa Watangazaji waliohama hapo  wakisema wanakosa Uhuru wanapokuwa kwenye Redio hiyo.

No comments: