Wednesday, September 17, 2014

BUNGE LA KATIBA LAZIDI KUPINGWA,LHRC NAO WATAKA LISIMAMISHWE MARA MOJA,SOMA TAMKO LAO HAPA


Mkurugenzi wa uwezeshaji na uwajibikaji wa kituo hicho  IMELDA URIO wakati akisoma tamko la kituo hicho kuhusu mwenendo wa mchakato wa katiba 
Ikiwa bado wadau mbalimbali nchini wakiendelea kupiga kelele kutaka bunge maalum la katiba lisimamishwe mara moja kwa kile wanachodai ni wizi wa fedha za watanzania ndani ya bunge hilo,nao Kituo cha sheria na haki za Binadamu  nchini LHRC wameibuka na kumtaka na Rais wa jamhuru ya muungano wa Tanzania kuchukua hatua mara moja ya kulisimamisha bunge hilo hadi maridhiano ya ukweli yatakapopatikana.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam na mkurugenzi wa uwezeshaji na uwajibikaji wa kituo hicho bi IMELDA URIO wakati akisoma tamko la kituo hicho kuhusu mwenendo wa mchakato wa katiba hadi hapa ulipofikia,ambapo amesema kuwa wamekuwa wakifwatilia kwa ukaribu mchakato huo na  kutoa maoni yao ambayo kwa kiasi kikubwa yamekuwayakipingwa kwa maslahi ya kisiasa.

Wanahabari wakisikiliza kwa makini

BI EMELDA anasema kuwa kumekuwa na kauli za kuwachanganya watanzania juu ya uwezo wa Rais kulivunja bunge hilo akitolea mfano kauli ya mwanasheria mkuu wa serikali aliyoitoa mnamo tarehe 17 mwezi wa nane kuwa Rais hana mamlaka ya kulivunja bunge hilo kwa madai ya kutokuwepo kwa kipengele cha sheria  ambapo amesema kuwa kauli hiyo haina maslahi wala uchungu wa watanzania ambao ndio walipa kodi zinazowalipa kodi wajumbe hao.

Aidha ametolea mfano kauli nyingine aliyoitoa mwenyekiti wa bunge hilo mh SAMWELI SITTA ambapo alisikika akisema kuwa pamoja na makubaliano ya kuahirisha bunge hilo hadi baada ya uchaguzi na kusema upigaji kura wa kifungu kwa kifungu uko pale pale pamoja na uwezekeno wa theluth mbili kutopatikana, huku akitaka kuwashirikisha watanzania walioko nje ya nchi,wagonjwa na wale walioko hijja, Kituo cha sheria wamesema kuwa mwenyekiti huyo anafanya hayo yote huku akijua wazi kuwa anapotosha umma.

Katika hatua nyingine LHRC wamesema kuwa swala la uchaguzi halihusiani kabisa na mchakato wa katiba mchakato wa katiba unaweza kabisa kuendelea na uchaguzi sambamba kwani rasimu ya katiba hususani ibara ya 268 inatoa kipindi cha mpito cha miaka minne kabla ya kuanza kutumia katiba mpya.hivyo kusitisha mchakato wa katiba kwa kisingizio cha uchaguzi ni kosa kubwa sana ambalo linatokana na kuwaachia wanasiasa mchakato huo ambapo wamesema kuwa wanasiasa kazi yao kubwa ni kuangalia maslahi yaoya kuwepo madarakani na si maslahi ya wananchi.


LHRC ni wadau wengine waliojitokeza kupinga mwenendo wa bunge hilo huku kukiwa na wimbi la watu mbalimbali wakiwemo wanasiasa,asasi za kiraia ambao nao wamekuwa wakitaka bunge hilo liahirishwe mara moja

No comments: