Mwenyekiti wa chama cha democrasia na maendeleo CHADEMA mh FREMAN MBOWE akizungumza wakati wa mkutano mkuu wa chama hicho jijini Dar es salaam leo |
Mwenyekiti
wa chama cha Democrasia na maendeleo CHADEMA mh FREMAN MBOWE ambaye pia ni
mwenyekiti wa wa umoja wa katiba ya wananchi UKAWA ametangaza maandamano na migomo ya nchi nzima
ambayo haina ukomo kwa kushiriakiana na umoja wa katiba ya wananchi UKAWA yenye
lengo la kupinga mchakato wa katiba mpya unaoendelea kwa sasa kwa madai kuwa ni
ubadhilifu mkubwa wa pesa za watanzania.
Akizungumza
jijini Dar es salaam Mapema leo wakati akifungua mkutano wa mwaka wa CHADEMA
mkutano ambao pia utamchagua mwenyekiti mpya wa chama hicho mh MBOWE amesema
kuwa umoja wa katiba ya wananchi ukawa wamechoshwa na mambo yanayoendelea ndani
ya bunge la katiba na sasa wameamua kuingia katika maandamano ili kushinikiza
wananchi kudai haki hao ambayo inachezewa na watu wachache.
“naomba
mnisikilize makamanda,sasa tumechoka na mazungumzo ambayo hayana
mwisho,tunadanganyana mchana kweupe,na mwisho wa siku tunamaliz a hela za
watanzania bila kupata muafaka wa maana,hivyo natoa maagizo kwa makamanda wangu
wa kila mkoa,sasa tunakwenda kufanya kitu ambacho kitaishtua
dunia,tutaandamana,tutafanya migomo ya kila namna,iwe kwa kibali cha polisi au
bila kibali ila yatafanyika”amesema mh MBOWE
Mh
MBOWE amesema kuwa lengo la maandamano hayo ni kumshinikiza mwenyeikiti wa
bunge la katiba Tanzania pamoja na serikali kulisitisha bunge hilo mara moja
kwa kile ambacho amedai kuwa linaendelea kuwaibia watanzania mali zao huku
wakijua kuwa bunge hilo haliwezi kuwapatia watanzania katiba.
Aidha mwenyekiti huyo amewashiomba wanachama wa
vyama vya upinzani wanaotoka mikoa jirani na DODOMA kuandamana na mabango
kuelekea bungeni kuzuia shughuli za bunge hilo,huku akiwaomba viongozi wa vyama
hivyo kuhakikisha kuwa wanaratibu maandamano hayo ambayo amesema kuwa yataanza
siku yoyote.
Aidha katika hatua nyingine mwenyekiti wa chama cha
wananchi CUF mh IBRAHIM HARUNA LIPUMBA
amesema kuwa umoja wa katiba UKAWA ni mpango wa mungu na lengo lao ni
kuwafungua macho watanzania ambapo amesema lengo lao ni kuimarisha ushirikiano
wao na ikibidi wasimamishe mgombea mmoja katika chaguzi zijazo.
Mkutano mkuu wa chama cha CHADEMA unafanyika leo
jijini dare s salaam ambapo lengo kubwa ni uchaguzi wa viongozi wa ngazi za juu
za chama hicho ikiwemo nafasi ya uenyekiti wa chama hicho ambayo inashikiliwa
na mh MBOWE.
Katika mkutano huo ulihudhuriwa na viongozi
mbalimbali wa kisiasa akiwemo makamu mwenyekiti wa CCM mh PHILIPO
MANGULA,mwenyekiti wa NCCR MAGEUZI mh JAMES MBATIA,mwenyekiti wa CUF mh IBRAHIM
LIPUMBA pamoja na mabalozi kutoka nchi mbalimbali duniani kwa hapa Tanzania.
No comments:
Post a Comment