Thursday, September 18, 2014

HABARI KUBWA LEO--MBOWE ASIMAMISHA JIJI LA DAR KWA MASAA ZAIDI YA MATANO,ATINGA POLISI NA WANASHERIA WAKE NA MAMIA YA WANACHAMA,PICHA ZAIDI ZIKO HAPA

Mmoja wa wanachama ambaye alibishana na askari na kujikuta akipata kibano kidogo na baadae kuachiwa
 Mwenyekiti wa chama cha democrasia na maendeleo CHADEMA  mh FREMAN MBOWE leo amefanya shughuli za jiji la Dar es salaam kusimama kwa muda baada ya kufika makao makuu ya polisi jijini akiwa na wanasheria wa chama huku mamia ya wanachama wake wakiwa nyuma yake kutaka kujua kinachoendelea hapo ikiwa ni kuitikia wito wa jeshi hilo waliomtaka kufika kwa maelezo zaidi.
Baada ya mh MBOWE kufika makao makuu ya polisi aliingia ndani na kuhojiwa zaidi ya masaa manne na kisha mwanasheria wa chama hicho mh TUNDU LISSU kutoka na kauli kuwa mwenyekiti huyo ametuhumiwa kuwa makosa ya uchochezi alioufanya juzi jumapili wakati akihutubia wanachama wake ambapo alisema kuwa wataandamana na kufanya migomo nchi nzima kupinga bunge la katiba linaloendelea.
Hata hivyo kwa taarifa ya TUNDU LISSU ni kuwa mh MBOWE ameachiwa kwa dhamana kwa ajili ya kusubiri kesi yake hiyo.
Hata hivyo mh MBOWE alionekana kufichwa sana kiasi cha kutoikuwa rahisi kuonekana na wafuasi wake
 Nje ya ofisi za jeshi la polisi wananchi ambao ni wafuasi wa CHADEMA walionekana kuwa na hamu ya kumwona mwenyekiti wao ambapo kwa mara kadhaa walisikika wakiimba na kupiga kelele ambapo polisi walianza kuwasukuma na kusogeza silaha zo karibu ila hali ikawa shwari.hadi mtendao huu unaondoka katika eneo la tukio wafuasi hao walikuwa wameondoka kwa maombi ya mwanasheria tundu lissu kuwa waondoke hapo ili kuepusha vurugu zisizo na msingi

Viongozi wa chama hicho walikuwepo kuhakikisha kuwa hali inakua shwari




Mh TUNDU LISSU akizungumza na wananchi pamoja na wanahabari ambao aliwataka kuondoka katika maeneo hayo ili kuepusha vurugu ambazo zingeweza kuwaharibia zaidi katika kesi hiyo



No comments: