Wednesday, September 17, 2014

HOT NEWZZ--CHADEMA WATANGAZA KUMSINDIKIZA MBOWE KESHO HADI MAKAO MAKUU YA POLISI ALIKOITWA,WANACHAMA NAO WATAKIWA KUJITOKEZAA

Mwanasheria mkuu wa CHADEMA akizungumza na wanahabari muda huu
 Chama cha democrasia na maendeleo CHADEMA leo kimetangaza kuwa mwenyekiti wao keshoi ataenda polisi makao makuu kuitikia woito wa jeshi hilo ambao ulikuja kwa barua ukimhitaji mwenyekiti huyo kufika makao makuu ya jeshi hilo.

Kauli hiyo imetangazwa muda huu makao makuu ya chama hicho na  wanasheria mkuu wa chama hicho mbunge TUNDU LISSU wakati akizungumzia wito wa jeshi la polisi kumhitaji mwenyekiti wao kwa kile ambacho ameadi kuwa hakijawekwa wazi wanamwitia nini.

"Tumepokea barua ya jeshi la polisi makao makuu wakimtaka mwenyekiti wetu kufika makao makuu ya polisi kwa maelezo,kamati kuu ya chama imeridhia mwenyekiti aende ila hawezi kwenda mwenyewe hivyo wanasheria wote wa chama walioko mkoani Dar es salaam watamsindikiza kwa ajili ya kujua mwenyekiti wetu ameitiwa nini.hivyo tunaomba wanasheria wote wa chama kesho tukutane polisi makao makuu saa tano kwa ajili ya kumsindikiza. 
Naibu katibu mkuu wa chama hicho JOHN MNYIKA akizungumza muda huu 
Aidha naibu katibu mkuu wa chama  hicho mh JOHN MNYIKA NAYE naye amewataka wananchi na wapenzi wa chama hicho kujitokeza kesho kumsindikiza mwenyekiti wao kwa ajili ya kusikiliza kile ambacho mwenyekiti wao ameitiwa nini na jeshi la polisi
HABARI KAMILI YA MKUTANO WA CHADEMA NA WANAHABARI LEO ITAKUJIA BAADAE

No comments: