Saturday, September 6, 2014

michezo--TIZAMA SIMBA ILIVYOWARARUA WAKENYA LEO TAIFA MBELE YA MAXIMO

Mshambuliaji mpya wa Simba SC, Mkenya Paul Kiongera akishangilia moja ya mabao yake mawili katika ushindi wa 3-0 jioni ya leo kwenye mchezo wa kirafiki dhidi ya Gor Mahia ya Kenya Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Chini ni mashabiki wa timu hiyo wakifurahia raha za Kiongera, mkali mpya wa mabao wa Msimbazi.


Vigogo wa kundi la Friends Of Simba SC, kushoto Zacharia Hans Poppe kulia Crescentius Johm Magori wakila raha Taifa leo

Mtu hatari mbele ya lango; Paul Kiongera kushoto langoni mwa Gor Mahia leo

Kocha wa Yanga SC (picha ndogo chini kushoto), Marcio Maximo kulia akiwa Msaidizi wake, Mbrazil mwenzake, Leonardo Leiva wakifuatilia mchezo wa kirafiki kati ya Simba SC na Gor Mahia ya Kenya jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Simba imeshinda 3-0. picha kubwa ni wachezaji wa Simba wakishangilia moja ya mabao yao leo.

No comments: