Thursday, September 18, 2014

MWANDISHI WA HABARI WA TANZANIA DAIMA ALIVYOPOKEA KIPIGO CHA POLISI WAKATI WA SAKATA LA MBOWE





NA KAROL VICENT

 SIKU moja kupita Baada ya Makamu wa Rais Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal kuvitaka Vyombo vya ulinzi kufanya kazi kwa ukaribu na Waandishi wa Habari,lakini sasa Jeshi la polisi limeipuuzia kauli hiyo na kuzidi kuwafanyia unyama waandishi wa Habari.
Hayo yameonekana Leo Jijini Dar es Salaam wakati waandishi wa Habari walipokuwa wakichukua taarifa za Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Freeman Mbowe alipokuwa polisi Makao makuu,
Ambapo Polisi walikuwa wakilinda ulinzi maeneo hayo walikuwa wakiwazuia waandishi na kuwafanyia unyama wa hali ya Juu ikiwemo kuwapiga hadi kuwapelekea maumivu katika sehemu mbalimbali za mwili.
 Akizungumza na Mwandishi wa Mtandao huu juu ya Unyama aliofanyiwa na jeshi la Polisi Mwandishi Mwandamizi wa Gazeti la Tanzania Daima Josephati Issango alisema anasikitika sana kwa Jeshi la polisi kumfanyia unyama huo huku wakijua yeye ni mwandishi
“hivi Jeshi la Polisi tumelikosea nini maana mimi hapa na peni na kitabu tu nachukua taarifa sasa  leo wananifuata na kunipiga tena wanivunja mguu,na kunipora vifaa vyangu nilivyonavyo kwa kosa lipi wakati kazi yangu mimi ni kuchukua taarifa tu”alisema Issango

No comments: