Tuesday, October 21, 2014

HII SASA INAWAHUSU WAANDISHI WA HABARI WOTE TANZANIA

Meneja wa udhibiti wa viwango kutoka baraza la habari Tanzania akizungumza na wanahabari mapema leo kuhusu mchakato wa tuzo za umahiri wa uandishi wa habari nchini Tanzania
 Baraza la habari Tanzania leo wametangaza rasmi kuanza kwa mchakato wa tuzo za umahiri wa uandishi wa habari Tanzania mashindano ambayo yatakjuwa ni mara ya sita kufanyika nchini Tanzania.

Akizungumza na wanahabari leo jijini dare s salaam Meneja wa udhibiti wa viwango  kutoka baraza la habari MCT Bi PILI MTAMBALIKE amesema kuwa katika mashindano ya mwaka huu kuna mabadiliko kidogo ambapo amesema kuwa kuna makundi ambayo yameongezwa katika nafasi zinazoshindaniwa ambayo ameyataja kuwa ni gesi,mafutana uchimbaji madini na kundi la afya ya mama na mototo.ambapo amesema kuwa makundi hayo yameongezwa kutokana na umuhimu wake hapa nchini kwa sasa.
 Tamasha hilo ambalo limepangwa kufanyika mwaka mwakani mwezi wa tatu tarehe 24,2015 ambapo mtambalike amesema kuwa tuzo hizi zinalenga kuwatambua na kuwatunza waandishi wa habari waliofanya kazi yao vizuri katika kazi zao na makundi mbalimbali kushindaniwa
Mmoja kati ya waratibu wa shindano hilo Bi CHIKU LWENO akiielezea mikakati ya tuzo hizo kwa msimu huu
Makundi yatakayoshindanishwa mwaka huu ni uandishi wa habari za uchumi,habari,michezo na tamaduni,mazingira,afya,watoto,HIV/UKIMWI,utawala bora,jinsia,sayansi na technologia,afya ya mama na motto,uchunguzi,elimu,watu wenye ulemavu,utalii na uhifadhi,mpiga picha gazeti,mpiga picha runinga,mchora katuni bora,uandishi wa habari za kilimo,afya ya uzazi kwa vijana,pamoja na tuzo ya uandishi wa habari za gesi,mafuta na uchimbaji madini,pamoja na kundi la wazi.

Bi PILI MTAMBALIKE amewataka waanndishi wa habari kujitokeza kwa wingi kupeleka kazi zao ili zishindanishwe na kupata mshindi wa tuzo hizo.

No comments: