Wednesday, December 3, 2014

CHADEMA WAPATA MWALIKO BUNGE LA ULAYA,SOMA HAPA

CHADEMA Waalikwa Bunge La Ulaya
Baadhi ya viongozi wa chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA wamepata  mwaliko wa kuhudhuria Bunge la ulaya nchini Ubelgiji, na kukutana na viongozi wa bunge hilo, pamoja na kuhudhuria mkutano Mkuu wa 27 wa  chama cha CDU nchini Ujerumani.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam Kaimu katibu Mkuu wa Chadema Zanzibar,  Salum Mwalim amesema, ujumbe huo wa CHADEMA utafanya mazungumzo na viongozi wa bunge hilo, juu ya mambo mbalimbali yanayoendelea hapa nchini.

Amesema  kama chama kikuu cha upinzani,  watakaowakilisha ni ujumbe wa viongozi wakuu wa Chadema na wamejipanga kufanya mazungumzo, maalumu kwa mustakabali wa taifa la Tanzania.

Aidha mwalimu amesema wakiwa  nchini ujerumani  viongozi hao watazungumzia changamoto  mbalimbali  zinazolikabili taifa
Ujumbe huo wa CHADEMA tayari umeshaanza safari yake, na utakuwa kwenye ziara hiyo kwa muda wa siku kum



No comments: