Saturday, December 13, 2014

CUF YALIA NA RAFU ZA UCHAGUZI, WANACHAMA WAO WANNE WATEKWA,WAMWANDIKIA BARUA WAZIRI MKUU PINDA


kaimu naibu katibu mkuu ambaye pia ni mkurugenzi wa mipango na uchaguzi SHAWEJI MKETOakionyesha barua ambayo wamemwandikia waziri mkuu juu ya rafu za uchaguzi
Ikiwa kesho ndo siku ya uchaguzi wa serikali za mitaa kufanyika nchini tanzaniachama chawananchi CUFleo kimesema kuwa kimemuandikia waziri mkuu pamoja na wizara ya tamisemibarua rasmi ya malalamiko juu ya rafu mbalimbali zinazochezwa juu ya wagombea wa chamachao pamoja na UKAWA kwa ujumla.
Akizungumza na wanahabari mapema leo  makao makuu ya chamahicho kaimu naibu katibu mkuu ambaye pia ni mkurugenzi wa mipango na uchaguzi SHAWEJI MKETO amesema kuwa kuna udhibitisho kuwa CCM kwa kushirikiana na serikali wamejiandaa kuvurugauchaguzi huo ili kupora ushindi ambapo amesema kuwa mkakati huo umeonekana wazi baada ya wagombea wengi wa UKAWAkuenguliwa katika kinyanganyiro hicho.
Amesema tukio la jana lililotokea mabibo jijini dare s salaam ambapo kura zaidi ya 500 zilikutwa zikichapishwa kwa ajili ya kutumika huko kilosa ni tukio ambalo limeonyesha wazi kwa hakuna mwenye nia ya dhati kulisaidia taifa kwani kinachofanyika ni wizi na wao kama chama hawawezi kuvumilia.
Mohamed Mnyaambunge akizungumzaambapo amesema kuwa baadhi ya kauli zinazotolewa na viongozi wa ccm asio nzuri ambapo ametolea mfano kauli ya kiongozi wa CCM NAPE NNAUYE kuwa yoyote atakayesumbua apigwe kabla ya kupelekwa polisi kauli ambayo aliiyoa katika kampeni za chama chake ni kauli ya kichochezi na yenye malengo ya fujo
Aidha akizungumzia matumizi mabaya ya nguvu za dolakatikachaguzi amesema kuwa jana wilayani tandahimba kata ya lokokoda wanachama wa cuf wapatao wanne walikamatwa na wanajeshi wa jeshi la wananchi JWTZ wakiwa wamewafuata majumbani kwao ambapo baada ya kuwakamata waliwaingiza katikakarandinga ambalo lilikuwa na sakari zaid ya 50 na kuwapeleka katika kambi ya jeshi ya naliendelele iliyopo mtwara ambapo askari wawili kati ya hao walianza kuwapiga kwa madai kuwa wameficha mabomu majumbani kwao,ambapo baadae kiongozi wa msafara aizuia wasipigwe na kuwapatia magodoro wakalala hadi asubuhi na kuwapeleka katika kituo cha polisi na kuwaacha kwa OCD kwa mahojiano.

Amesema kuwa matendo haya hayaji kwa bahati mbaya kwani yanalenga kuwadhoofisha wanachama na wanachi ili wasijitokezekwawingi katika vituo vya kupiga kura ilikuwachagua viongozi wanaowataka.
Cuf
wameitaka serikali kuacha mara moja jaribio la kuingiza nchi katika machafuko yasiyo na tija kwa kuwawatanzania ni watu wa amani na amani yetu haiwezi kuchezewa na watu wachache kwa tamaazao zamadaraka.

No comments: