Monday, March 31, 2014

MAGAZETI YOYE YA LEO JUMANNE APRIL 1 2014 HAYA HAPA.KARIBUNI MPATE HABARI

.
.
.
.
.
.

HABARI AMBAYO IMELISONONESHA TAIFA LEO--------AJALI MBAYA 14 WAFARIKI DUNIA, WAOKOAJI NAO WAZOLEWA WAFARIKI NA KUFIKIA WATU 21



         Watu 21 wamefariki dunia katika ajali mbaya imetokea Wilaya ya Rufiji, mkoani Pwani ikihusisha magari 3 na wengine 11 kujeruhiwa.Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, ACP Ulrich Matei, alisema ajali hiyo imetokea katika Barabara Kuu ya Dar es Salaam-Lindi, eneo la Ikwiriri, wilayani humo.
         
        Awali ajali hiyo ilihusisha magari mawili, Toyota Hiace (T 948 CUX), iliyokuwa ikitokea Ikwiriri kuelekea Rufiji ambalo lilikwenda kukwaruzana na Lori(T 132 AFJ) kwa nyumba, ambalo lilikuwa limeharibika na kusimama barbarani.

HEKA HEKA ZA UBUNGE HUKO CHALINZE---MWENYEKITI WA CCM AHAMIA CHADEMA

Mgombea ubunge wa chadema huko chalinze akizungumza na wanahabari jimboni huko

Ramadhan Idd Kisebengo Mwenyekiti wa CCM Kata ya Kidaula akijivua gamba na kukabidhiwa kadi ya CHADEMA baada ya mkutano wa hadhara uliofanyika Chalinze mjin

wapiga kura tunaelewana au mvua kali

MECHI YA AZAM, SIMBA YAINGIZA MIL 26/-



Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Azam na Simba iliyochezwa jana (Machi 30 mwaka huu) Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam imeingiza sh. 26,455,000.
 
Watazamaji 4,741 walikata tiketi kushuhudia pambano hilo ambapo Azam iliibuka na ushindi wa mabao 2-1. Viingilio vilikuwa sh. 5,000, sh. 15,000 na sh. 20,000.

Mgawanyo kwa mapato ulikuwa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) sh. 4,035,508.47, gharama za kuchapa tiketi sh. 3,908,686 wakati kila klabu ilipata sh. 5,460,687.63.

Uwanja sh. 2,776,620.83, gharama za mechi sh. 1,665,972.50, Bodi ya Ligi sh. 1,665,972.50, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 832,986.25 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 647,878.19.

HELIOS TOWERS LAUNCHES IN BUILDING SOLUTIONS (IBS)

Helios Towers Chief Executive Officer, Norman Moyo (L) addressing participants the official launching of Helios In Building Solution in Dar es Salaam at the weekend. With him are some of Helios Tanzania staff members. .

Helios Towers Chief Executive Officer, Norman Moyo (R) exchanging ideas with  OGM Consultancy Principal  Architect, Oswald Modu (L)  during the official launching of Helios In Building Solution in Dar es Salaam at the weekend. Lookingt on is AWD Ltd MD, Jamaal Awadh.

Some of invitees exchanging views during the launching event. 



            THE telecoms Infrastructure Company in Tanzania, Helios Towers has inaugurate the In-Building Solutions (IBS) to strength and magnifying telecommunication networking in Tanzania.


            Speaking during the launching of the operation in Kilimanjaro Hyatt Regency hotel in Dar es Salaam, yesterday the Chief Executive Officer of Helios Towers Norman Moyo said, this is new services in Tanzania that will ensure good and reliable telecoms networking in big and tall building in the country as well as strong telecoms road in the country.


PICHA TATU ZINAZOONYESHA JINSII POLISI LEO WALIVYOWAKUSANYA BODA BODA WALIOKUWA WANAINGIA KATIKATI YA JIJI

Habari24 leo ilifanikiwa kunasa juhudi za jeshi la polisi katika kuwaondoa bodaboda ndani ya jiji la dar es salaam ambapo picha za juu zinaonyesha walivyokuwa wanakusanywa muda mfupi uliopita katikati ya jiji,hatua hiyo inakuja kutekeleza agizo la mkuu wa mkoa wa dar es saal said meck sadick la kutaka bodaboda kutoingia ndani ya jiji na badala yake waishie nje ya jiji

Sunday, March 30, 2014

MAGAZETI YA LEO JUMATATU MARCH 31, 2014 HAYA HAPA YOTE



BREAKING NEWZZ--DARAJA LA MTO RUVU MVUA YASABABISHA MAJANGA MUDA HUU


HABARUI AMBAZO TUMEPENYEZEWA HAPA NI KUWA MVUA KUBWA INAYONYESHA MAENEO MBALIMBALI YA TANZANIA IMESABABISHA DARAJA LA MTO RUVU LINALOUNGANISHA MSATA NA BAGAMOYO KUFUNIKWA NA MAJI KIASI CHA KUTAKA KUVUNJIKA MAGARI YOTE YANAYOTUMIA DARAJA HILO YAMETAKIWA KUPITA CHALINZE KWANI HALI YA DARAJA HILO NI MBAYA

HABARI AMBAYO INATIKISA NCHI----KARIAKOO YAHAMIA COCO BEACH KWA MUDA,YALE MAONYESHO MAKUBWA YA WAFANYABIASHARA WA KARIAKOO YANAENDELEA MUDA HUU.CHUKUA MUDA WAKO KUFAIDI KINACHOENDELEA HUKO

Wateja mbalimbalia ambao habari24 blog imewanasa asubuhi ya leo jumapili wakiwa tayari wanafaya shoping zao ndani ya maonyesho hayo ambayo yanafanyika katika ufukwe wa coco beach,maonyesho ambayo yameandaliwa na kampuni ya HAZINA CAPITALlakini kupata udhamini mkubwa wa mtandao wa TIGO TANZANIA

Bidhaa ambazo huwa unazipata ndani ya soko la kariakoo sasa zinapatikana ndani ya ufukwe wa coco beach kwa gharama nafuu sana na bidhaa nzuri kwa utulivu kabisa


wauzaji wa bidhaa hizo wakiwa wanaweka mambo sawa asubuhi hii wakati wakijiandaa kuwahudumia mamia ya wateja wa dar es salaam watakaojaa muda sio mrefu ndani ya coco beach

Saturday, March 29, 2014

MAGAZETI YOTE YA LEO TAREHE 30 MWEZI WA TATU JUMAPILI HAYA HAPA

.
.
.
.

KITUKO KUTOKA CHALINZE--BARA BARA MBOVU ZAKWAMISHA KAMPENI ZA CHADEMA KWA MASAA KADHAA,MGOMBEA UBUNGE MATHAYO TORONGEY AJITOSHA KUCHIMBA BARABARA MAMBO YAENDE,CHEKI HAPA

Panaitwa Kidung'hwe, Kata ya Msoga kwao mkulu...hakuna barabara kuna kile ambacho kinaitwa mapitio ya mifugo.

Imebidi mgombea ubunge mathayo torongei kuingia kazini ili kuokoa jahazi baada ya msafara wao kukutana na miundominu mibovu ya barabara ya chalinze wakati wakienda kwenye kampeni za uchaguzi mdogo huko chalinze
Mathayo torongei kiwa kazini

BAADA YA YULE MWANDISHI WA DAILY MAIL KUITWA TANZANIA,HATIMAYE AWAGEUKA WALIOMWITA,AANDIKA MAKALA NYINGINE YA KUKOSOA TENA JK NA NYALANDU JUU YA UJANGILI


Mwandishi huyo akitembelea hifadhi ya meno ya tembo
           



NA KAROL VICENT



          KILE kinachotafsriwa ni kugeukwa kwa serikali ya Tanzania na Mwandishi wa Gazeti la Sunday Mail la Nchini uingereza  Martini Fletcher baada ya kuandika makala nyingine ikihishutumu tena serikali ya Jakaya kikwete kwa kushindwa kuwachukilia hatua Majangili.

        Kugeukwa kwa Serikali ya Tanzania kumetokana na Serikali ya Tanzania kupitia Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu kutumia Garama kubwa ya  kumuita Mwandishi huyo kile kinachoonekana ni kujikosha kwa serikali baada ya mwandishi huyo kuandika makala ikiituumu serikali ya Tanzania kushindwa kuwachukulia hatua Majangili.


HAYA SASA---DK SLAA NA MAKATIBU WA VYAMA VYA UPINZANI WAUNDA UKAWA NJE YA BUNGE,WATANGAZA KUFANYA MIKUTANO MIKUBWA NCHI NZIMA KUPINGA MCHAKATO WA KATIBA MPYA,KESHO WANAANZIA MWANZA,SOMA HAPA

Makatibu wakuu wa vyama vya CHADEMA,CUF,NA NCCR MAGEUZI wakizungumza na wanahabari jijini dar es salaam baada ya kutangaza muungano wao wa kupinga mambo ambayo yanaendelea bunge maalum la katiba

     Mungano wa vyama vitatu vya upinzani vyenye wabu nge bungen ambao kwa sasa unajiita umoja wa katiba ya wananchi UKAWA leo umetangaza kufanya mikutano ya hadhara kiwa mikoa yote Tanzania kupinga kile ambacho wanakiita kuhujumiwa kwa mchakato wa kupata katiba mpya ambao wanaituhumu moja kwa moja ccm kuwa wanataka kuhujumu mchakakato wa kupata katiba mpya.

              Akitangaza maamuzi hayo ambayo ni ya makatibu wakuu wa vyama vya CUF,NCCR MAGEUZI NA CHADEMA,katibu mkuu wa CHEDEMA dk WILBROD SLAA wakati wa mkutano na wanahabari katika katika makao makuu ya CHADEMA amesema kuwa ukawa imekuwa ikifanya kazi ndani ya bunge na sasa wameunda UKAWA nje ya bunge ili kuwasaidia wale waliopo bungeni kuwaletea watanzania katiba ya wananchi na siyo ya ccm.

          Dk SLAA anasema kuwa UKAWA NJE  wameamua kuwafuata wananchi wa Tanzania kuwaunganisha nguvu zao na kuwaeleza ukweli juu ya mchakato wa katiba mpya unavyotekwa na ccm na kufanya wabunge wa bunge maalum la katiba wanaotaka katiba ya wananchi kuonewa ndani ya bunge na kutokutendewa haki katika bunge hilo.

          Anasema kuwa UKAWA  NJE watafanya mikutano ya hadhara nje na ndani kwa nchi nzima ambapo kampeni hiyo wametangaza kuizindua kesho mkoani mwanza na baadae kufanyika kila mkoa wa Tanzania.

Katibu mkuu wa CHADEMA DK WILBROD SLAA akizungumza kwa niaba ya makatibu wakuu wenzake katika mkutano na wanahabari jijini dar es salaam muda mfupi uliopita

TAARIFA KWA VIJANA WOTE DAR ES SALAAM NA TANZANIA


BAVICHATAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo yenye jukumu la kusimamia sekta ya Vijana nchini imeandaa Kongamano la Vijana kutoka Vyuo vya Elimu ya Juu kuhusu Wajibu wa Vijana katika Kuimarisha Muungano Wetu Miaka 50 tangu kuzaliwa kwake. 

Friday, March 28, 2014

CHEKA NA UJIFUNZE NCHI YAKO


MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI 29, MARCH 2014

.
.
.
.

TAZAMA PICHA ZA ENEO LA JANGWANI BAADA YA MVUA KUNYESHA

PICHA HIZZI MBILI ZINAONYESHA MADHARA YA MVUA ILIYONYESHA USIKU WA LEO HADI ASUBUHI JIJINI DAR ES SALAAM NA KUFUNIKA NYUMBA ZOTE ZA MAENEO YA JANGWAANI

TAZAMA MAFURIKO MAENEO YA JANGWANI BAADA YA MVUA YA LEO

 Hivi ndivyo maji yanavyo onekana kujaa katika makazi Jangwani

 Baadhi ya watu wakionekana nje baada ya maji kuingia ndani

 Muonekano wa nyumba pamoja na njia ndogo ndogo zikiwa zimejaa maji 

Picha na Husein wa Dar es salaam yetu Blog
- See more at: http://msikecorner.blogspot.com/2014/03/tazama-mafuriko-maeneo-ya-jangwani.html?spref=fb#sthash.EYvbaJ19.dpuf

TAZAMA MAFURIKO MAENEO YA JANGWANI BAADA YA MVUA YA LEO

 Hivi ndivyo maji yanavyo onekana kujaa katika makazi Jangwani

 Baadhi ya watu wakionekana nje baada ya maji kuingia ndani

 Muonekano wa nyumba pamoja na njia ndogo ndogo zikiwa zimejaa maji 

Picha na Husein wa Dar es salaam yetu Blog
- See more at: http://msikecorner.blogspot.com/2014/03/tazama-mafuriko-maeneo-ya-jangwani.html?spref=fb#sthash.EYvbaJ19.dpuf

EXCLUSIVE---JUKWAA LA KATIBA LATANGAZA NIA YAKE YA KWENDA DODOMA KULIFUNGA BUNGE MAALUM LA KATIBA IWAPO TU-----------

Mjumbe wa jukwaa la katiba tanzania bw izrael ilunde akizungumza katika kutano huo na wanahabari juu ya uamuzi wa jukwaa la katiba kuhusu bunge la katiba tanzania


              Jukwaa la katiba Tanzania JUKATA leo limetangaza nia yake ya kutaka kuwashawishi wananchi kuandamana hadi mjini Dodoma kulifunga bunge la katiba endepo kama hawataridhika na bunge hilo na kama watagundua kuwa wabunge hao hawana nia ya dhati ya kuwapatia katiba bora wananchi.
      
         Hayo yamesemwa leo muda huu jijini dar es salaam na kaimu mwenyekiti wa jukwaa hilo bw HEBRON  MWAKAGENDA wakati akizungumza na vyombo mbalombalo vya habari kuhusu mwenendo wa bunge hilo maalum la katiba linaloendelea mjini Dodoma.

Kaimu mwenyekiti wa jukwaa la katiba tanzania bw HEBRON MWAKAGENDA akizungumza na wananchi muda mfupi uliopita kuhusu bunge la katiba


                 MWAKAGENDA anasema kuwa jukwaa la katiba linaendelea kutathmini kile kinachoendelea bungeni na kama wakijiridhisha kuwa kinachoendelea hakielekei kuwapatia watanzania katiba mpya bali ni upotevu wa muda na rasimali za taifa basi JUKATA itatumia ibara ya nane ya katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania kuwaongoza wananchi kulifunga bunge maalum la katiba na kuanza harakati za  kuitafuta katiba mpya kwa utaratibu wenye mantiki na tija kwa taifa.
             
          Aidha jukwaa la katiba Tanzania limeipinga vikali hotuba iliyotolewa na raisi wa Tanzania dk JAKAYA KIKWETE wakati akifungua bunge hilo ambapo wamesema kuwa  hotuba ile ilifaa sana kutolewa na mwenyekiti wa chama cha siasa kwenye mkutano wa chama husika na sio katika bunge kama lile.
               
        Bw MWAKAGENDA anasema kuwa jukwaa la katiba linapenda kuwataarifu watanzania wote kwa ujumla kuwa katiba inayotengenezwa sio ya chama chochote cha siasa bali ni y watanzania wote hivyo ni kosa kwa chama cha siasa kuuteka mchakato huo kama wao ndo wanatengeneza katiba yao ambapo anasema kitendo cha wanasiasa kuwa na sauti kubwa katika bunge la katiba kimeufanya mchakato wote kutekwa na kuonekana kama mchakato wa kisiasa.

          Mchakato wa bunge la katiba unaendelea huku kukiwa na mabishano maengi ambayo watanzania wengi wamekuwa wakishindwa kuelewa ni ya nini hadi kufikia matumizi ya matusi na vijembe kutawala katika bunge hilo