Friday, October 31, 2014

MPYA KUTOKA CCM LEO

Katibu
wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na waandishi wa habari
kwenye ukumbi wa Sekretarieti,makao makuu ya Chama Ofisi Ndogo Lumumba
jijini Dar es Salaam.
HABARI KAMILI

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimepokea kwa furaha Chama cha Frelimo kuibuka na ushindi katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 15, mwaka huu.


Katika uchaguzi huo, aliyekuwa mgombea kwa tiketi ya Frelimo, Mhe Filipe Nyusi ameibuka kidedea na sasa ndiye Rais Mteule wa Msumbiji ambaye baada ya kuapishwa atashika mikoba itaakayoachwa na Rais anayemaliza muda wake, Armando Gwebuza.

KUTOKA TFF LEO


 




Makocha 35 wameteuliwa kushiriki kozi ya ukocha ya Leseni C ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) itakayofanyika mjini Morogoro kuanzia Novemba 5 hadi 19 mwaka huu.

Kozi hiyo itaendeshwa na Mkufunzi wa CAF, Sunday Kayuni na itafanyikia Mchikichini College ambapo washiriki wote wanatakiwa kuwasilisha vyeti vyao vya ukocha vya ngazi ya Kati (Intermediate) pamoja na vyeti vya kitaaluma vya elimu ya sekondari (academic).

samahani kwa picha inayohuzunisha--AJALI MBAYA MTO WAMI MUDA HUU

HABARI ZA HIVI PUNDE...

Ajali mbaya daraja la Wami basi la Simba Mtoto na Lori baada break za Lori kufeli, 
Dereva wa Lori amepoteza maisha hapohapo...
Habari ambazo tumepenyezewa hapa kutoka daraja la wami ni kuwa lori moja  moja limefel breck na kuvaana na basi la simba mtoto maeneo hayo na kusababisha kifo cha dereva wa lori hilo

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI: GADNER. G. HABASH ATUA RASMI EFM



Mtangazaji mahiri Gardner.G. Habash,amejiunga na kituo cha Radio kinachokuja kwa kasi hivi sasa EFM 93.7 cha jijini Dsm ili kuongeza nguvu katika kikosi chao.

Akizungumza leo na waandishi wa habari afisa habari wa EFM Kanky Mwaigomole amesema wameamua kumchukua Gardner kwasababu ni

miongoni mwa watangazaji hodari nchini mwenye kipaji cha hali ya juu hivyo kuongeza chachu ya mafanikio katika kituo hicho kipya.

“Gardner ataendesha kipindi kiitwacho Ubaoni kuanzia saa tisa alasiri mpaka saa moja kamili jioni kuanzia Jumatatu ya tarehe 03 mwezi wa 11 mwaka huu”alisema Kanky.

Gardner alimaarufu “KAPTENI” alianza kazi na kituo cha Radio Clouds fm na baadaye Times fm ambapo kwa sasa ametua Efm akitanguliwa na wakongwe kama Dj Majey,Dizzo One,Sos B,Denis Ssebo,Maulidi Kitenge,Omari Katanga,Scholastica Mazula na Kanky Mwaigomole

MSIBA--HUYU NDIYE MTANGAZAJI MAARUFU ALIYEFARIKI LEO TANZANIA

Mtangazaji wa zamani wa Radio Tanzania Dar es salaam(RTD) ambayo sasa ni TBC Taifa, Ben Hamis Kikoromo au maarufu Ben Kiko (pichani) amefariki duania.

Mwandishi huyo mkongwe nchini Ben Kiko amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika hosptali ya taifa ya rufaa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu. 

Ben Kiko alihamishiwa katika hosptali ya Muhimbili kutokea hosptali ya Jeshi ya Milambo ya mkoani Tabora ambako alilazwa kwa ajili ya matibabu ya figo kwa muda wa wiki mbili. 

VIONGOZI WA MSONDO WAMTEMBELEA RAIS KIKWETE IKULU


D92A1988
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akipiga picha ya pamoja  na viongozi wa Bendi ya Msondo ngoma ikulu jijini Dar es Salaam leo mchana.Viongozi hao walimtembelea Rais Kikwete ikulu leo na kufanya naye mazungumzo(picha na Freddy Maro)

Tuesday, October 28, 2014

MAGAZETI LEO JUMATANO OCTOBER 29,2014 YAPO HAPA

1_e5dda.jpg
2_02e53.jpg

AMKA NA PICHA HII--SIASA HAIKOSI VITUKO

Hapa ndipo tunapofikia hatua ya kusema kuwa ukipenda kitu unaweza kuwa kama mwenda wazimu,vijana wanne ambao juzi katika mkutano wa kusaini makubaliano ya ukawa katika viwanja vya jangwani walionekana vivutio baada ya kuingia wakiwa wamejichora miili yao na rangi za chama cha democrasia na maendeleo chadema na kuwaacha watu waliokuwa pale hoi kwa mshangao mkubwa .nimependa uamke kwa kuitizama picha hii mdau wangu 

HIVI NDIVYO MSANII CHID BENZ ALIVYOPANDISHWA KIZIMBANI KWA KOSA LA KUDAKWA NA UNGA

 Msanii wa Hip Hop, Rshid Makwiro ‘Chidi Benzi’ akisindikizwa na askari Polisi wakati akiingia katika chumba cha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini leo Dar es Salaam kujibu mashtaka matatu likiwemo la kukutwa na dawa za kulevya kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. (Picha na Francis Dande)

MSANII
wa Muziki wa Kizazi Kipya (bongo fleva), Rashidi Abdallah Makwaro (29),
maarufa kama Chid Benz, amefikishwa mahakamani akikabiliwa na mashitaka
matatu ikiwemo kukutwa na Dawa za kulevya aina ya Heroin yenye thamani
ya Sh. 38,638, bangi ya Sh. 1,720 na vifaa ya kuvutia dawa hizo kijiko
na kigae.

HUYU NDIYE MCHEZAJI BORA WA MWEZI HUU LIGI KUU TANZANIA BARA


Kiungo wa timu ya Azam, Salum Abubakar amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa mwezi Oktoba wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) inayoendelea kutimua vumbi kwenye viwanja mbalimbali nchini.

Abubakar ambaye pia ni mchezaji wa timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) aliwashinda wachezaji wengine 20, huku wanne kati ya hao wakichuana naye kwa karibu.

Wachezaji hao ni Joseph Mahundi wa Coastal Union, Salim Mbonde (Mtibwa Sugar), Rashid Mandawa (Kagera Sugar) na Najim Magulu wa JKT Ruvu Stars.

Kwa kuibuka mchezaji bora, Abubakar atazawadiwa kikombe na fedha taslimu sh. milioni moja kutoka kwa wadhamini wa ligi hiyo kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom.

Jopo maalumu la makocha waliopo katika viwanja vyote vinavyotumika kwa mechi za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) ndiyo wanaofanya kazi ya kuchagua mchezaji bora kwa kila mechi kwa kuzingatia vigezo vilivyowekwa, na baadaye alama zao kujumlishwa ili kumpata mshindi wa mwezi.



Monday, October 27, 2014

MAGAZETI YA LEO JUMANNE OCTOBER 28,2014 YAKO HAPA

1_c6516.jpg
2_ee901.jpg

SERIKALI IPO NJE YA NCHI,RAIS KIKWETE VIETNAM MH PINDA OMAN ZIARANI

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  akizungumza na Naibu Waziri Mkuu wa Oman, Mheshimiwa Sayyid Fahad Mahmoud Al Said  baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa  wa Kimataifa wa Muscat wa  Royal Airport  kwa ziara ya siku mbili ya kikazi nchini humo 

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa  na mwenyeji wake Rais Mhe
Truong Tan Sang wa Vietnam  wakati wa mapokezi yake rasmi katika Ikulu
ya Hanoi katika siku ya kwanza ya ziara yake rasmi  ya siku mbili
nchini humo 

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete na mwenyeji wake Rais Mhe Truong
Tan Sang wakikagua gwaride la heshima lililoandaliwa kwa ajili yake
wakati wa mapokezi yake rasmi katika Ikulu ya Hanoi katika siku ya
kwanza ya ziara yake rasmi  ya siku mbili nchini humo

TAMASHA KUBWA LA TIGO WELCOME PACK LAFANA JIJINI ARUSHA.PICHA ZIKO HAPA

 Wasanii wa kikundi cha Ngoma cha Manyara Group  Mkoani Arusha kikiwapa burudani wakazi wa mkoa huo waliofurika kwenye uwanja wa Sheikh Amri Adeid mwishoni mwa wiki kushuhudia tamasha la Tigo welcome pack, Kampuni ya Tigo imeanzisha kifurushi cha welcome pack kitakachomwezesha mtumiaji wa Tigo kupata muda wa maongezi wa dakika 20, mb175,sms bila kikomo na pesa shilingi mia 500 kwenye akaunti yake ya tigopesa, yote hayo kwa shilingi 1000 mteja atakaponunua laini yake ya Tigo.



Wasanii wa kikundi cha Original Komedi kikiwapa burudani wakazi wa mkoa wa Arusha waliofurika kwenye uwanja wa Sheikh Amri Adeid mwishoni mwa wiki kushuhudia tamasha la Tigo welcome pack, Kampuni ya Tigo imeanzisha kifurushi cha welcome pack kitakachomwezesha mtumiaji wa Tigo kupata muda wa maongezi wa dakika 20, mb175,sms bila kikomo na pesa shilingi mia 500 kwenye akaunti yake ya tigopesa, yote hayo kwa shilingi 1000 mteja atakaponunua laini yake ya Tigo.
Msanii Ibrahim Mussa Maarufu Roma Mkatoliki akiwapa burudani wakazi wa mkoa wa Arusha waliofurika kwenye uwanja wa Sheikh Amri Adeid mwishoni mwa wiki hii ni moja ya sehemu  burudani zitolewazo kwenye kampeni ya kifurushi kipya cha Tigo cha welcome pack. Kampuni ya Tigo imeanzisha kifurushi cha welcome pack kitakachomwezesha mtumiaji wa Tigo kupata muda wa maongezi wa dakika 20, mb175,sms bila kikomo na pesa shilingi mia 500 kwenye akaunti yake ya tigopesa, yote hayo kwa shilingi 1000 mteja atakaponunua laini yake ya Tigo.

Meneja wa mauzo wa Tigo Mkoani Arusha Bw. Aidan Komba akiongea na wananchi waliojitokeza kwa wingi kwenye tamasha kubwa la Tigo welcome pack uwanja wa Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha mwishoni mwa wiki.

Mmoja kati ya watu waliojitokeza kwenye tamasha la welcome pack akipokea zawadi toka kwa mfanyakazi wa Tigo.

Msanii Joseph Haule maarufu kama Professor J akiwapa raha wakazi wa mkoa wa Arusha waliofurika kwa wingi kwenye tamasha la welcome pack uwanja wa Sheikh Amri Adeid mwishoni mwa wiki hii ni moja ya sehemu  burudani zitolewazo kwenye kampeni ya kifurushi kipya cha Tigo cha welcome pack.

HABARI KUBWA JIJINI--ACT WAWAUNGA MKONO UKAWA,WAMWAGA PONGEZI KWA MUUNGANO WAO,NAO KUZUNGUKA NCHI NZIMA KUHAMASISHA KURA YA HAPANA KWA KATIBA

Katibu mkuu wa chama cha ACT TANZANIA--SAMSON MWIGAMBA akizungumza na waandishi wa habari ofisi za chama hicho kijitonyama jijini dar es salaam muda huu kuhusu mambo mbalimbali katika chama hicho
Ikiwa imepita siku moja tangu umoja wa katiba ya wananchi UKAWA kusaini makubaliano ya kuunganisha vyama vyao kwa lengo la kuwa na nguvu zaidi ya kisiasa katika chaguzi zijazo nacho chama kipya katika siasa za Tanzania cha ACT-TANZANIA  kimeibuka na kupongeza hatua hiyo na kuunga mkono harakati hizo za kisiasa za kuunganisha nguvu ya upinzani kwa kusema kuwa kufanya hivyo itawasaidia kukiangusha chama cha mapinduzi kirahisi huku akitoa tahadhari kwa muungano huo.

 Akizungumza na wanahabari muda huu katika ofisi za chama hicho kuhusu maadhimio ya mkutano wa kamati kuu ya chama hicho katibu mkuu wa ACT Samson mwigamba pamoja na kutokuweka wazi kuwa chama chake kipo tayari kujiunga na UKAWA amesema kuwa ni hatua nzuri kwa siasa za upinzani kama muungano huo utakuwa ni muungano wa sera na kutetea wananchi huku akisema chama chake kitaungana na chama ambacho kipo tayari kuwatetea wanachi na sio kwa ajili ya kuiangusha CCM ili wagawane madaraka ya serikali.

“Muungano wa ukawa ni hatua nzuri katika siasa  ila tunatoa tahadhari sana kwa muungano huo usije ukawa ni muungano wa kugawana madaraka, sisi tutaungana na yeyote ambaye yupo tayari kuwatetea wananchi ila hatutaungana na watu ambao watakuwa wanataka kuiangusha CCM ili kuingia ikulu na kugawana madaraka”Amesema MWIGAMBA.

Aidha akizungumzia katiba iliyopendekezwa katibu mkuu huyo amesisitiza kile ambacho na UKAWA walisisitiza kwa kusema kuwa katiba iliyopendelezwa ni wizi na udanganyifu mkubwa kwa wananchi ambao umefanywa na chama cha mapinduzi hivyo nao wanatangaza rasmi kuzunguka nchi nzima kuwahamasisha wananchi wote kupiga kura ya hapana kwa katiba iliyopendekezwa kwa kile walichodai kuwa haijakidhi mahitaji nya watanzania kwa sasa.

“Chama cha ACT kwa nia moja tumeamua kuzunguka kwa watanzania wote kuhamasisha kura ya hapana kwa watanzania na zoezi hilo litaanza mara moja kwa kuwa katiba hii iliyopendekezwa haijakidhi matarajio  na maoni ya watanzania wote.

Akikizungumzia cha hicho kipya amesema kuwa ACT kitazinduliwa rasmi tarehe 5 december mwaka huu jijini Dare s salaam ambapo kwa mujibu wa katiba ya chama hicho kutafwatiwa na mkutano mkubwa wa hadhara wa uzinduzi wa chama hicho ambao utafanyika jijini mwanza.
SOMA TAMKO LAO LOTE HAPA----

Sunday, October 26, 2014

MAGAZETI YA LEO JUMATATU OCTOBER 27,2014,HABARI,MICHEZO NA UDAKU


.
.
.
.
.
.
.

CCM NAO WALIUNGURUMA HUKO ZANZIBAR KIBANDAMAITI JANA,PICHA ZIKO HAPA

unnamed3
Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein na Mke wa Makamo wa Pili wa Rais Mama Pili Balozi wakiwa katika Mkutano wa Hadhara katika Viwanja vya Demokrasia Kibanda maiti Mjini Unguja leo uliohutubiwa na Rais wa Zanziba r na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyeekiti CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein  .[Picha na Ikulu.]

HUU HAPA MKATABA WA UKAWA WALIOSAINI LEO


YAMETIMIA UKAWA--HII NI HISTORIA YA SIASA ZA TANZANIA,CHEKI PICHA ZA KUSAIN MAKUBALIANO HAPA


Historia kubwa imewekwa muda huu hapa viwanja vya jangwani jijini dar es salaam Tanzania Ambapo vyama vinavyounda umoja wa katiba ya wananchi ukawa muda huu wamesain mkataba ambao unawafanya wao sasa kuungana na kuzungumza lugha moja ya kuhakikisha kuwa wanafika mbali zaidi wakiwa pamoja,umoja huo ambao unaundwa na CHADEMA,CUF,NCCR MAGEUZ pamoja na NLD muda huu wamesaini kwa pamoja makubaliano hayo mbele ya wanachama wao maelfu waliojitokeza katika viwanja hivyo hapa jijini dar es salaam.
Akizungumza na wanachi waliojitokeza hapa katibu mkuu wa chadema aesema kuwa makubaliano hayo sio makubaliano ya vyama na viongozi wakuu bali ni makubaliano ya wanachi wote ambao wanapenda haki na amani ya tanzania.
mtu wangu hapa kuna picha za shuguli hiyo ya kusaini makubaliano hayo na tutazidi kukupa kile kinachojiri hapa uwanja wa jangwani.
Wenyaviti wa vyama hivyo kwa pamoja wakisaini makubaliano hayo ambayo yanawaweka pamoja na kufanya siasa ya Tanzania kuingia katika historia nyingine kubwa na ambayo haijawahi kutokea
Mamia ya wanachama waliojitokeza hapa
Naibu katibu mkuu zanzibar chaderma salum mwalim akizungumza lugha ya tatu.
PICHA NYINGINE ZA TUKIO HILI ZIKO CHINI HAPO

PICHA 14 ZA AWALI HISTORIA WANAYOWEKA UKAWA LEO VIWANJA VYA JANGWANI ZIKO HAPA


Watanzania wengi sana waliojitokeza hgapa katika viwanja vya jangwani wakitaka kushughudia tukio la kihistoria katika siasa za Tanzania ambapo inasemekana kuwa vyama vinavyounda umoja wa katiba ya wanachi Tanzania UKAWA leo watasaini makubaliano rasmi ya kushirikiana katika chaguzi zote zinazokuja
Hapa nimekuwekea picha za awali za tukio hilo ambalo linaendelea hapa viwanja vya jangwani na litarushwa na ITV pamoja na vituo vingine vingi,
tutakuletea tukio nzima baadae hapa hapa mtu wangu






Saturday, October 25, 2014

KUTOKA UKAWA LEO

Kuna taarifa ambazo bado hazijawa na uhakika sana kuwa umoja wa katiba ya wananchi UKAWA kesho ndio siku ambayo watasaini makubaliano makubwa ya kusimamisha mgombea mmoja katika kila chaguzi zinazokuja mbeleni,habari hizi awali zilitangazwa na umoja huo wiki iliyopitya ambapo walisema kuwa tarehe 26 mwezi huu ndio siku ambayo watasaini makubaliano hayo japo hawakutaja mahali halisi ila walisema watasaini mbele ya watu katika mkutano mkubwa wa hadhara,taarifa zisizo rasmi zinasema kuwa mkutano huo ni kesho katika viwanja vya jangwani na utakuwa ukirushwa live na Television mbili za Tanzania ,bado hatujahakikisha hilo ila tunakuahidi kukupa ukweli wa taarifa hiyo na kama ni kweli basi tutakuletea tukio hilo kesho,ASANTEN

WAZIRI MKUU PINDA YUPO ZIARANI POLLAND


PG4A6770
PG4A6747
PG4A6721