Friday, January 9, 2015

VURUGU ZA KUAPISHWA VIONGOZI WA MITAA,CUF WAIBUKA TENA,SOMA WALICHOSEMA LEO

Naibu katibu mkuu wa CUF bi MAGDALENA SAKAYA akizungumza na wanahabari mapema leo makao makuu ya chama hicho juu ya uapishwaji wa viongozi wa serikali za mitaa unaoendelea nchini
 Chama cha wananchi CUF kimetangaza kulaani vikali zile wanazoziita vurugu na  hujuma wanazodai zinafanywa  na chama cha mapinduzi CCM katika zoezi la uapishwaji wa viongozi wa serikali za mitaa linaloendelea nchi nzima.
Akizugumza na wanahabari mapema leo Naibu katibu mkuu wa chama hicho bi MAGDALENA SAKAYA amesema kuwa mkakati wa ccm ulianza katika zoezi la uchaguzi huo katika kubatilisha matokeo ambayo chama cha CUF kilishinda na sasa CCM imeamua kutumia mbinu chafu ya kutaka kuwaapisha viongozi wao ambao hawakushinda katika matokeo ya uchaguzi huo.
Wanahabari mbalimbali wakisikiliza kwa makini
Akitaja maeneo kadhaa ambayo wagombea wa CUF walishinda lakini wasimamizi wa uchaguzi wakashindwa kuwatangaza na badala yake kuwapeleka viongozi wa CCM kwenda kuapa kuwa ni mtaa wa mwinyimkuu kata ya mzimuni kinondoni ambapo mgombea wa cuf HASSAN ABUBAKARY alishinda katika uchaguzi huo lakini msimamizi wa uchaguzi huo aliitisha uchaguzi mwingine uchaguzi ambao uligomewa na wanachi na badala yake akatangazwa mgombea wa CCM, FUNUA ALLY kuwa ndiye mshindi.


Mtaa mwingine ni mtaa wa ukwamani kata ya kawe ambapo mgombea wa cuf alishinda lakini fomu za ushindi hazikusainiwa hadi leo na badala yake mgombea wa ccm ndiye ametangazwa mshindi. Aidha maeneo mengine ambayo amesema yamefanyika mchezo huo ni mtaa wa msisiri kata ya mwananyamala,mtaa wa kiwalani kata ya migombani,mtaa wa kigogo fresh,pamoja na mtaa wa malapa,kinyerezi,migombani,bunda mara,pamoja na maeneo mengine ambayo wanachi wanazidi kurepoti tukio hilo.

Aidha bi SAKAYA amesema kuwa kutokana na uchakachuaji huo mkubwa ni wazi kuwa lazima viongozi waliohusika ikiwa ni pamoja na mkurugenzi wa uchaguzi wa kinondoni na waziri husika wawajibike kwa kuachia nafasi zao mara moja kwani ni aibu kwa taifa kuwaibia wanachi kwa kiasi hicho.

Aidha amekionya chama cha mapinduzi kwa kile alichosema hii ni mipango yao ya kuiviuruga Amani ya Tanzania kuwa nguvu ya umma waliyokutana nayo uchaguzi huu itakuwa ni Zaidi katika uchaguzi ujao hivyo mbinu chafu hazitavumilika hata mara moja.

Kumeshughudiawa vihoja katika zoezi la kuapishwa viongozi wa serikali zaa mitaa jijini Dar es salaam ambapo katika ukumbi wa landmari pamoja na kule ilala  juzi kulizuka fujo kubwa baada ya kugundulika kuwa kuna viongozi ambao hawakushinda ila walipewa barua za kwenda kuapishwa jambo ambalo wanachi hawakuliafiki na kusababisha fujo kubwa.

No comments: