Vuguvugu la Urais ndani ya umoja wa Katiba ya Wanachi UKAWA linazidi
kushika kasi kufuatia Mwenyekiti wa CUF prof. Ibrahim Lipumba kufungua
pazia la kupelekwa jina lake UKAWA ambapo Mwenyekiti wa Chama cha NLD,
Dk Emmanuel Makaidi naye ametuliwa kuingia katika kinyang’anyiro cha
kugombea urais ndani UKAWA.
Mwenyekiti wa Chama cha NLD, Dk Emmanuel Makaidi amesema tayari
chama chake kimeshapendekeza jina lake kuwa miongoni mwa vigogo
watakaoshindanishwa kwenye kinyang’anyiro hicho ili lipatikane jina moja
litakaloiwakilisha UKAWA kupambana na chama tawala cha Mapinduzi.
Aidha, makubaliano ya umoja huo yanaelekeza vyama kupendekeza jina
moja litakalowakilishwa katika Kamati ya Wataalamu ya Ukawa kabla ya
kushindanishwa na majina mengine.
Kwa upande wa Vyama vya NCCR Mageuzi na Chadema bado havijaonyesha
mwelekeo wa kupatikana jina la mgombea wa urais kutokana na michakato
inayoendelea ndani ya vyama hivyo.
No comments:
Post a Comment