Monday, February 9, 2015
HABARI KUBWA--BARCELONA KUTUA BONGO MWEZI UJAO
Mshambuliaji wa zamani wa FC Barcelona na timu ya Taifa ya Uholanzi Patrick Kluivert alizungumzia ujio wa magwiji FC Barcelona nchini mwezi wa tatu mbele ya waandishi wa habari kwenye mgahawa wa Sports Lounge uliopo jijini Dar Es Salaam ,Pembeni ya Kluivert ni mwenyekiti wa DRFA Ndugu Almas Kasongo. Magwiji hao wa Barcelona wanataraji kucheza na wachezaji nyota wa Tanzania kwenye uwanja wa Taifa mnamo mwezi wa machi tarehe 28.
Timu ya wachezaji nyota wa zamani wa Barcelona FC watacheza na wachezaji wa zamani wa Tanzania, Tanzania All Stars Machi 28 kwenye uwanja wa Taifa jijini.Mwakilishi wa wachezaji wa zamani wa Barcelona, Patrick Kluivert alisema jana kuwa mechi hiyo itawahusisha wachezaji nyota wa Barcelona wakiwemo, Edgar Davids, Gaiza Mandieta, Ludovic Giuly, Francesco Coco na wengine wengi waliopitia klabu hiyo kwa miaka tofauti.Kluivert alisema kuwa kikosi chao kina wachezaji nyota ambao ni maarufu duniani na wanaamini mechi itakuwa nzuri na yenye ushindani mkubwa.
Alisema kuwa yeye ni mwenyeji sana hapa Tanzania kwani huu ni ujio wake wa tatu na anaamini kuwa jinsi mashabiki wanapenda sana mpira wa miguu, itakuwa fursa kubwa kwao kuona vipaji vya zamani ambavyo vimetukuka.“Ninafurahi kuja nchini Tanzania kwa mara ya tatu, ni faraja kubwa pia kucheza hapa nchini kwa mara ya kwanza, naomba mashabiki wa soka wajae uwanjani kuona mpira wenye ushindani,” alisema Kluivert.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment