Ni miezi michache imesalia kabla ya Tanzania kuingia katika zoezi nzito sana la
uchaguzi mkuu wa Rais Wabunge na madiwani ambapo Tanzania inatarajia kupata Rais
mpya kabisa.
Wakati tukisubiri kwa hamu kubwa kuona ni nani
atachukua kijiti cha rais aliyeko madarakani tayari watu mbalimbali wameanza
kuonyeha nia ya kukitaka kiti hicho ambapo tumeshughudia watu mbalimbali
wakitangaza nia wazi wazi kuwa wanaitaji nafasi hiyo kwa hudi na uvumba huku
wengine wakifanya mambo yao kimya kimya ila lengo ni kupata nafasi ya kugombea
na hatimaye kupata nafasi ya kuwa rais watanzania.
Pamoja na nafasi hiyo kubwa ya urais pia majimbo ya
uchaguzi nayo yapo katika purukushani kuhakikisha yananyakuliwa na wengine
wakifanya kila liwezekanalo kulinda nafasi zao za ubunge katika majimbo yao.
Moja kati ya jimbo ambalo sasa limeanza kupiganiwa
ni jimbo analoongoza mwenyekiti wa chama cha democrasia na maendeleo chadema
ambaye pia ni mwenyekiti mwenza wa umoja wa katiba ya wananchi UKAWA mh FREMAN
MBOWE ambapo vijana kadhaa kutoka chama cha mapinduzi CCM wameanza kuonyesha
nia mbalimbali za kutaka kumngoa mbunge wa jimbo la hai katika nafasi yake
hiyo.
Katika pitapita za mtandao huu katika mitandao mbalilimbali
tumeshughudia kijana ambaye amekuwa akitangaza nia ya kugombea ubunge katika jimbo
la hai kwa tiketi ya chama cha mapinduzi
CCM katika uchaguzi ujao huku akiwa
tayari anasambaza mabango katika mitandao kana kwamba ni muda wa kampeni la
yote hii ni mwendelezo wa kutangaza nia.rejea picha ya
juu.
Katika uchaguzi wa
mwaka huu unatabiriwa kuwa na ushindani wa aina yake kutokana na watu kujiandaa
kwa kina kuakikisha kuwa wanaangoa watu katika majimbo yake lakini wabunge nao
kupigania nafasi zao za kuyaongoza majimbo yao kwa miaka mingine mitano.
Mtandao huu utakuwa
ukikupa kila kinachojiri katika harakati hizi za uchaguzi mwanzo mwisho.
No comments:
Post a Comment