Mwenyekiti wa muda wa chama cha ACT TANZANIA kadawi limbu akizungumza na wanahabari mapema leo Jijini Dar es slaam |
NA KAROLI VINSENT NA EXAUD MTEI
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe ameingia
kwenye kashfa nzito,baada ya kudaiwa kumuhonga pesa Msajili wa Vyama vya
Kisiasa nchini ili kuhumjumu Mwenyekiti
Halali wa Chama cha ACT-Tanzania Kadawi Limbu ili aondolewe kwenye Nafasi hiyo
ili apewe Zitto Kabwe.
Zitto
Kabwe ambaye uanachama wake ndani ya Chama cha Demokrasia Cha Chadema umebakia
kwenye makaratasi baada ya kufukuzwa na
uongozi wa Juu wa chadema kwa madai ya kuandaa mipango ya kumuhuju mwenyekiti
wa chama hicho Freeman Mbowe.
Akifichua
Shutuma hizo,Mwenyekiti halali wa Chama cha ACT-Tanzania Kadawi Limbu leo
Jijini Dar es Salaam,wakati wa Mkutano na Waandishi wa Habari ambapo Limbu
akizungumza kwa Uchungu amesema inasikitisha kuona ofisi ya msajili wa
vyama vya siasa nchini ikizorotesha hususani vya upinzani kwa kuruhusu kuhongwa na
Zitto Kabwe.
Kwa upande wake Katibu mkuu Msadizi wa Chama cha ACT-Tanzania upande wa Bara Leopold Mahona akizungumza |
“Jamani
hili ni jambo la hatari sana mimi leo limbu ni mwenyekiti halali wa ACT
nashangaa sana kumuona msajili wa kisiasa anashirikiana na watu ambao mimi nawaona
ni majambazi wa siasa nchini wakiongozwa na zitto kabwe kuja kunihujumu mimi
ili nitoke kwenye nafasi niliyokuwanayo ,kiukweli sikubali najua wazi kabisia
na ushahidi uko wazi kwamba Zitto kabwe amemuhonga Msajili ili mimi nitoke
“Amesema limbu.
Limbu ameongeza kuwa kitendo cha msajili huyo
kusema uongozi wake ulikuwa batili kumtimu anayejiita Katibu halali wa
ACT-Tanzania Samsoni Mwigamba kwenye nafasi aliyokuwa nayo ni uwongo wa hali ya
juu ambao unashusha hazi ya ofisi ya msajili nchini.
“Kikao tulichotumia kumfukuza Mwigamba na Profesa Mkumbo kilikuwa halali
tena hata kanuni zinaturuhusu wazi kutoa hukumu lakini nashangaa sana ,leo
msajili anakuwa upande wa majambazi wa siasa wakiongozwa na zitto kabwe katika
kuniondoa mimi lakini najua huyu, msajili ananini na mimi?”amehoji Limbu.
Aidha,Mwenyekiti
huyo wa Zamani wa Chama cha ADC amendelea kumtupia lawama msajili huyo na kusema
hatoweza kukubali kuwaachia anaodai ni wahuni wenye nia ya kuubomoa upinzani
nchini wa huku wakishirikiana na chama cha mapinduzi CCM.
“mimi
sijawai kuona katika maisha yangu, utoto huu
unaofanywa na hawa wakina
mwigamba na wenzake kwani sababu kubwa ya wao kutaka mimi niondoke ACT ni
kukataa mipango ya kukifanya chama hichi cha ACT kuwa ni CCM B na kuubomoa
upinzania nchini na kukiweka Chama cha Chadema kuwa Adui wa ACT na mimi
nilipokataa wao wakajifanya kugombana na mimi na kuandaa mipango ya kuniondoa
ACT”
No comments:
Post a Comment