Tuesday, February 10, 2015

NAPE ATEMBELEA MAJIRA LEO

 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye (kushotia), akisalimiana na Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya Bussines Times, Imma Mbuguni, alipowasili katika Ofisi za kampuni hiyo jijini Dar es Salaam,  akiwa katika mwendelezo wa ziara ya vyombo vya habari aliyoaianza wiki iliyopita .
 Nape akimsalimia Meneja Uhusiano wa Bussines Times Ltd, Julieth Lamosai, baada ya kutambulishwa kwake na Mbunguni wakati wa ziara hiyo
 Nape akienda na Mbunguni kwenye ukumbi kwa ajili ya mazungumzo

 nape akisalimiana na Mkurugenzi wa Kiwanda cha Uchapaji cha Bussines Times (BTL), Omari Holaki baada ya kuwasili ukumbini kuzungumza na uongozi wa kampuni hiyo
Mtahiriri wa Majira Eckland Mwaffisi (kulia) na Mhariri Mtendaji wa Kampuni hiyo, Imma Mbuguni, wakiwa tayari kumsikiliza Nape ukumbini wakati wa ziara hiyo.
 Meneja Biashara wa BTL Lecil Moshi akiluliza swali ili kupata ufafanauzi kutoka kwa Nape wakati wa kikao chake na uongozi wa kampuni huyo.
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye (kulia) akizungumza na uongozi wa Kampuni ya Bussines Times, Wachapichaji wa Magazeti ya Majira, Bussines Times na Sports Starehe, akiwa katika mwendelezo wa ziara ya vyombo vya habari aliyoaianza wiki iliyopita mjini Dar es Salaam. Kushoto ni Mtahiriri wa Majira Eckland Mwaffisi na Mhariri Mtendaji wa Kampuni hiyo, Imma Mbuguni.
 Meneja Usambazaji wa BTL,  Sophia Mshangama akiuliza ni namna gani CCM kama chama tawala kimejenga misingi ya kushirikiana na wadau katika masuala ya kuinua uchumi, wakati ziara hiyo. Kushoto ni Mhariri wa Sport Starehe. Charles Mateso
 Baadhi ya wafanyakazi wa BTL wakimsikiliza Nape wakati wa ziara hiyo
 Baadhi ya wahariri wakimsikiliza Nape alipozungmza nao wakatai wa ziara hiyo
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye (kulia) akisisitiza CCM kuendelea kuimarisha ushirikiano na uwazi na vyombo vya habari, mwishoni mwa mazungumzo yake na wahariri wa magazeti ya kampuni ya BTL,  Wachapishaji wa Magazeti ya Majira, Bussines Times na Sports Starehe,  Wapili kushoto ni Mtahiriri wa Majira Eckland Mwaffisi na Mhariri Mtendaji wa Kampuni hiyo, Imma Mbuguni. Picha zote na Bashir Nkoromo)

No comments: