Thursday, February 12, 2015

RED ARROWS FC KUWEKA KAMBI TANZANIA.

Kutoka kushoto ni Ofisa habari wa Red Arrows  Lt Melody Siisii, Mwenyekiti wa Red Arrows Col Nolasco Chilando, Katibu Mkuu wa TFF Selestine Mwesigwa na Ofisa Ubalozi wa Zambia nchini Tanzania Alex Chila, wakiwa ofisi za TFF - PPF Tower leo.


Klabu ya Red Arrow FC inayoshiriki Ligi Kuu nchini Zambia inatarajiwa kuwasili jijini Dar es salaam-Tanzania jumatatu ya wiki ijayo kwa ajili ya kuweka kambi ya mafunzo ya wiki moja kujindaa na msimu mpya wa Ligi Kuu nchini humo 2015.

Uongozi wa klabu hiyo chini ya mwenyekiti wake Col Nolacso K Chilando ulifika leo makao makuu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Tanzania - TFF sambamba na Afisa habari wa klabu Lt Col Melody Siisii, Bw Alex Chila ofisa ubalozi wa Zambia nchini Tanzania kujitambulisha uwepo wao nchini.


Wakiongea na katibu  mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Tanzania - TFF Selestine Mweisgwa, uongozi wa timu hiyo umesema maandalizi ya kambi yameshakamilika na kikubwa walikua wanaliomba Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini kutambua uwepo wao na kuwasaidia kupata viwanja vya kufanyia mazoezi.

Naye Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini -TFF Bw.Mwesigwa  alisema wameyapokea maombi hayo ya Red Arrow FC  na kuwakaribisha nchini kwa ajili ya kambi yao na kusema ujio wao utafungua milango kwa vilabu vingine pia kuja kuweka kambi nchini.

Timu ya Red Arrow FC inayomilikiwa na jeshi la Anga nchini Zambia ikiwa nchini kwa mafunzo, inatarajia kucheza mchezo mmoja wa kirafiki na imeliomba Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini kuwatafutia timu moja ya kucheza nayo.

IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF

No comments: