Thursday, February 19, 2015

USIKOSE PIA HII KALI KUTOKA VINGUNGUTI LEO

Wananchi wa maeneo ya vingunguti wakifurahi pamoja na kamishna wa polisi kanda maalum ya Dar es salaam mara baada ya uzinduzi wa kituo hicho cha polisi leo
Kamishna SULEMAN KOVA akiwa na mdau ambaye ndiye aliyejengenga kituo hicho IMTIYAZ ABBAS wakizindua rasmi kituo hicho
Jeshi la polisi kanda maalum ya Dar es salaam leo wamezindua kituo kipya cha polisi kilichopo vingunguti jijini Dare s salaam ikiwa ni hatua ya kupambana na makundi ya wahalifu katika maeneo hayo ambayo yamekuwa sugu kwa sasa.

Kituo hicho ambacho kina uwezo wa kuhudumia zaidi ya wananchi million moja kimejengwa na mzalendo mkazi wa maeneo hayo IMTIYAZI ABBAS kituo ambacho kimegharimu zaidi ya shilingi za kitanzania million 56 hadi kumamilika kwake.

Akizungumza wakati wa kuzindua kituo hicho kamishna wa kanda maaluim ya Dar es salaam SULEMAN KOVA amesema kuwa kuwepo kwa kituo hicho saa ni ishara tosha kuwa uhalifu katika maeneo hayo umefikia tamati kwani kituo hicho kitakuwa na askari wa kutosha kuwahudumia wananchi wa maeneo hayo na viunga vyake.
 “sasa muda umefika wa wezi na wakabaji kutafuta kazi zingine za kufanya katika maeneo haya kwani tumejipanga kuhakikisha kuwa hakuna mhalifu atakayeishi katika maeneo haya,bora atafute kazi nyingine ya kufanya kama kulima kuliko kuendelea kuwa mhalifu”alisema kova
Kamishna kova amesema kuwa ni muda mrefu sasa wananchi wa maeneo hayo ya vingunguti wamekuwa wakilia kwa kukosa kituo bora cha polisi na sasa muda umefikia na wamepata kituo hicho sasa kilichobaki ni kushirikiana na wananchi kuwafichua wahalifu katika maeneo hayo.

Aidha amemshukuru mtanzania mzalendo ambaye ndiye aliyejitoa kwa pesa kujenga kituo hicho ambapo kamishna kova amewaomba watanzania wengine wazalendo kujitkeza kujenga vituo vya polisi ili kuwasaidia wanachi kupata usalama zaidi.
Aidha bwana ABBAS ambaye ndiye aliyejenga kituo hicho ameahidi kukiboresha zaidi ikiwa ni pamoja na kununua vifaa vya kisasa ili kuwasaidia askari katika kupambana na wahalifu.

Nao wanachi wa maeneo hayo ya vingunguti wameonyesha furaha yao baada ya kupata kituo hicho baada ya kukiriokuwa kumekuwa na wahalifu wengi sana katika maeneo hayo lakini ujio wa kituo hicho katika maeneo yao kitasaidia kupunguza uhalifu uliokithiri kttika maeneo hayo.
PICHA NYINGINE ZAIDI ZIKO CHINI

No comments: