Thursday, February 12, 2015

VITA INGINE DAR KESHO --CUF vs POLISI,VIJANA WA CUF WATANGAZA KUANDAMANA,KOVA ASEMA ATOKE MTU AKIONE CHA MOTO

Mwenyekiti wa jumuiya ya vijana ya chama cha wanachi CUF(juvicuf) HAMIDU BOBANI akizngumza na wanahabari kuhusu maandano hayo ya kesho
 Jumuiya ya vijana ya chama cha wananchi CUF (JUVICUF) leo wametangaza kufanya maandamano ya Amani siku ya kesho ijumaa maandamano ambayo yataanzia katika maeneo ya buguruni na kuelekea katika ofisi za wizara ya mambo ya ndani na baadae kuelekea tume ya taifa  uchaguzi Tanzania.

Akizungumza na wanahabari mapema leo mwenyekiti wa jumuiya hiyo HAMIDU BOBAN amesema kuwa maandamano hayo yana lengo la kupinga na kulaani vikali nguvu na uvunjaji wa haki za binadamu unaofanywa na jeshi la polisi lakini pia lengo lingine ni kufikisha malalamiko yao kwenye tume ya uchaguzi juu ya uchache wa siku zilizowekwa za uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura.

Amesema kuwa jumiya hiyo ilipeleka ombi la kufanyika kwa maandamano hayo jeshi la polisi lakini cha kushangaza ni kuwa viongozi wao waliitwa na polisi na kuambiwa kuwa haiwezekani kufanyika kwa maandamano hayo kwa sababu kuwa watasababisha usumbufu kwa wananchi wa kawaida ambao watakuwa katika shughuli zao jambo ambalo mwenyikiti huyo amesema kuwa sio sababu ya kutosha ya kufanya maandamanop hayo yasiwepo.

Amesema kuwa pamoja na jeshi la polisi kupiga marufuku maandamano hayo wao kama chama wanatangaza kuwa maandano hayo yapo kama kawaida na hakuna mtu wa kuyazuia na watafanya maandanao ya Amani lakini kama polisi wataanzisha vurugu wao watatumia njia za kujihami jambo ambalo litazua vurugu Zaidi.

Maandanamo hayo ambayo yataongozwa na waziri wa miundombini na uchukuzi wa serikali ya umoja wa kitaifa zanzibari mh JUMA DUNI HAJI ambaye tayari yupo jijini Dar kwa ajili ya maandano hayo wamepanga kuanza mnamo saa nne kamili asubuhi ambapo mwenyikiti huyo amewataka vijana wa chama chake kujitokea kwa wingi katika maandanao hayo.
KOVA APIGA MARUFUKU
Kamishna wa polisi kanda maalum Dar es salaam SULEMAN KOVA akizungumza na wanabari muda huu kupiga marufuku maandano hayo.

Jeshi la polisi kanda maalum ya Dar es salaam kupitia kamishina wa kanda hiyo SULEMANI KOVA limatangaza kuzuia maandamano yaliyopangwa kufanywa na jumuiya ya vijana ya chama cha wananchi cuf kwa kile walichodai kuwa sababu za kufanyika kwa maandamano hayo hazitoshi na badala yake itakuwa ni mbinu ya kuvuruga Amani katika jiji la Dar es salaam

Akizungumza na wanahabari masaa machache baada ya vijana wa CUF kutangaza kuwepo kwa maandamano hayo kamishna KOVA amesema kuwa maandamano hayo sio halali na hayana Baraka za polisi hivyo wananchi wasidanganyike kutoka kwani yanaweza kuwakuta makubwa na wasipate wa kuimlalamikia.
Amesema kuwa sababu zilizotolewa za kufanya maandanao hayo ni sababu ambazo zinajadilika hata bila maandanao hivyo haoni haja ya kufanya maandano hayo na badala yake akawashauri vijana hao kutafuta njia nyingine ya kuwasilisha malalamiko yao na sio kuandamana.

“Mimi nasema hakuna maandamano kesho na nashauri mtu yeyote asitoke kuandama kwa maana yatakayomkuta asije akamlaumu mtu atajikuta yupo sero bila sababu ya msingi,bora hawa vijana wakae majumbani kwao watafute njia nyingine za kufikisha maoni yao”amesema kova
Kamishna KOVA amesema kuwa polisi wamezuia maandamano hayo kwa nia nzuri chini ya kifungu cha 43(1-6) cha sheria ya polisi na polisi wasaidizi sura ya 322 kama ilivyorekebishwa mwaka 2002.

Aidha amesema kuwa kutokana na taarifa kuwa vijana hao wa CUF bado wanazidi kuhamasishana kufanya maandamano hayo inaonyesha wazi kuwa lengo ni uvunjifu wa Amani hivyo polisi watatumia uwezo wake wote hapo kesho kuhakikisha kuwa wanazima maandano hayo.


No comments: