Sunday, March 15, 2015

KOCHA MARSH KUAGWA LEO MUHIMBILI

        Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu wa nchini TFF, Mh. Jamal Malinzi ametuma salamu za ramirambi kwa familia ya Marsh kufuatia kifo cha kocha wa Taifa ya vijana Sylvester Marsh kilichotokea jana jijini Dar es salaam
Katika salam zake kwa familia ya marehemu, Mh. Malinzi amesema familia ya mpira wa miguu nchini TFF imeshtushwa na msiba huo na kusema Shirikisho na Taifa limempoteza mtu muhimu katika mpira wa miguu nchini.
Mwili wa marehem Marsh utaagwa leo saa 6 kamili mchana, katika kanisa la Hospital ya Taifa Muhimbili na kutasafirishwa kuelekea Igoma jijini Mwanza kwa mazishi majira ya saa 8 kamili mchana kwa bus dogo (coaster) laTFF.
  
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

No comments: