Friday, April 17, 2015

BARAZA KUU LA UONGOZI CUF LAMPA USHAURI RAIS KIKWETE

Baraza kuu la uongozi la taifa ndani ya chama cha wananchi CUF limemtaka         Rais wa wajamhuri ya muungano wa Tanzania Dk JAKAYA KIKWETE kukaa kwa pamoja na wadau wa uchaguzi nchini hususani vyama vya siasa kujadili kwa pamoja hali ya uandikishwaji wa daftari la ludumu la wapiga kura kutokana na sintofahamu inayoendelea nchini.

Akisoma maadhimio ya baraza hilio  lililokaa kwa siku mbili jijini Dar es salaam mwenyekiti wa chama hicho profesa IBRAHIMU  LIPUMBA amesema kuwa baraza hilo limesikitishwa sana na kasi ndogo ya uandikishwaji wa daftari la kudumu la wapiga kura kwa mfumo wa BVR ambapo mpaka sasa tume haijamaliza zoezi hilo kwa mkoa mmoja wa njombe jambo ambalo amesema sio ishara nzuri kuelekea uchaguzi mkuu Mwaka huu..


Amesema hali iliyopo sasa inaonyesha ishara mbaya hali inayoweza kusababisha kuahirishwa kwa uchaguzi mkuu ujao kwa sababu hali ya vifaa vya uandikishaji bado ni ndogo na hakuna jitihada za makusudi za kurekebisha hali hiyo.
Ameongeza kuwa tume ya taifa ya uchaguzi ilianzisha mchakato huo bila kutengewa fedha za kutosha za kununulia vifaa kuajiri na kuwapa mafunzo wafanyakazi watakaotumia mashine hizo,pamoja na kutoa elimu kwa wananchi juu ya umuhimu wa zoezi hilo hali ambayo imeathiri mchakato huo kwa kiasi k,ikubwa.

Aidha amesema kuwa huu sio muda wa kuzidi kutupiana mpira bali sasa ni muda wa raisi KIKWETE kuingilia kati zoezi hilo na kukubali kuwasikiliza wadau mbalimbali wa uchaguzi ili kwa pamoja washauriane nini cha kufanya ili uchaguzi mkuu uwepo katika tarehe iliyopangwa.
Katika hatua nyingine baraza hilo limeunga mkono maadhimio ya umoja wa katiba ya wananchi UKAWA ya kutoshiriki katika kura ya maoni juu ya katiba pendekezwa kwa kile walichoita kuwa haina maoni ya wananchi na haina faida kwa mtanzania wa kawaida.

No comments: