Wednesday, April 15, 2015

WAZIRI KIVULI WA ELIMU ACHARUKA,NI SAKATA LA CHAKULA MASHULENI,SOMA ALICHOKISEMA

Waziri kivuli wa elimu na mafunzo ya ufunzi mh SUZAN LYIMO akizungumza na wanahabari leo juu ya mambo mbalimbali yanayoikabili nchi kwa sasa hususani secta ya elimu nchini
 Waziri kivuli wa elimu na mafunzo ya ufundi mh SUZAN LYIMO ameitaka serikali iwebajibe ikiwa ni pamoja na kuhakikisha vyakula vya kutosha vinafika mashuleni badala ya kutaka  kuwawajibisha walimu wakuu ambao wamezuia wanafunzi wao kurudi mashuleni kwa sababu za upungufu wa chakula kwani kufanya hivyo ni kuwaonea kwa sababu walikuwa hawana njia mbadala ya kutatua tatizo hilo.
Akizugumza na wanahabari leo makao makuu ya chama cha Democrasia na maendeleo chadema Mh SUZAN LYIMO amewapongeza walimu wakuu ambao wamewazuia wanafunzi wao kurudi mashuleni baada ya likizo ya pasaka kutokana na kutokuwa na chakula katika shule zao hatua ambayo amesema ni ya kijasriri nay a kmupongezwa kwani wasingefanya hivyo wanhewez kuwasababishia wanafunzi matizo mengine kama ya migomo baada ya kukosa vyakula mashuleni.
Amesema kuwa yeye kama kama waziri kivuli wa elimu na mafunzo ya ufundi amekuwa akifwatilia swala hilo kwa umakini na amefika hadi wizara ya TAMISEMI kutaka kupata majibu kuhusu jambo hilo lakini amesema majibu aliyoyapata hayaridhishi kulinganisha na ukubwa wa tatizo husika.

Aidha amesema kuwa amezungumza na walimua wakuu ambao wamezifunga shule zao kutokana na ukosefu wa chakula ambapo amesema kuwa walimu hao wamekana kuzifunga shule na badala yake walichofanya ni kuongeza muda wa likizo kwa wanafunzi wao ili kusubiri uwezekano wa kupata chakula kwa ajili ya wanafunzi hao kinyume na madai ya serikali kuwa kuna walimu wamezifunga shule kinyume na sheria.

Katika sakata hilo ambalo linaendelea shule mbalimbali nchini zikiwemo malangali,mpwapwa,chanwe,ihungo,na nyingine nyingi zimeendelea na likizo ya pasaka ili kusubiri uwepo wa chakula katika shule hizo.
Katika hatua nyingine waziri huyo kivuli amesikitishwa sana na mfumo mbovu wa kuwapata walimu katika vyuo mbalimbali nchini kwa mwka huu ambapo tofauti na miaka mingine wanafunzi wamekuwa wakienda mafunzo ya vitendo kwa wiki zaidi ya tano lakini mwaka huu wanafunzi wa ualimu wamehudhuria mafunzo ya vitendo kwa wiki tatu tu kwa sababu ambazo zimetajwa kuwa ni kutokuwa na fedha za kutosha kuwapeleka wanafunzi hao kwa wiki nane mfulilizo.
Amesema kuwa kwa mfumo huo ni lazima tanzania itazidi kuporomoka kwa elimu kwa kuwa ni bora kuwa na majengo mabovu lakini serikali iwe na walimu wenye ujuzi wa kutosha kuwafundisha wanafunzi wake kwani kinyume na hapo kutazidi kuwa na anguko kubwa la elimu.

No comments: