Saturday, April 18, 2015

ZIG ZAG RALLY 2015 KUANZA KUTIMUA VUMBI MEI 3,MWAKA HUU HUKO TANGA

Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano
hayo,Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano hayo, Mehul Asher akizungumza
leo ofisini kwake,Picha na Mpiga Picha Wetu
NA MWANDISHI WETU, TANGA.
MASHINDANO ya mbio za Magari ya “Zig Zag Tanga Rally 2015”
yanatarajiwa kuanza kutimua vumbi mkoani Tanga Mei 3 mwaka huu
mzunguko wa pili kwenye yale ya Kitaifa chini ya ufadhili wa Zig Zag.
Mashindano hayo watashindanisha umbali wa km 135 na yatakuwa na awamu
tano, yatakayoanzia katika hotel ya Tanga Beach Resort na kupitia
maeneo ya Pongwe, Mkanyageni na Mjesani na kurudi yalipoanzia.
Akizungumza leo na waandishi wa habari, Mwenyekiti wa Kamati ya
Mashindano hayo, Mehul Asher alisema kuwa maandalizi yanaendelea
vizuri ambapo washiriki kutoka maeneo mbalimbali hapa nchini.
Alisema kuwa madereva watakaoshiriki katika michuano hiyo wanatazamiwa
kutoka mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Morogoro, Dar es Salaam, Tanga
ikiwemo wengine kutoka nchi za Kenya na Uganda.
Mwenyekiti huyo alisema kuwa mashindano hayo msimu huu yatakuwa na
upinzani mkubwa kutokana na barabara watakazotumia washiriki ni nzuri
hivyo itaweze kuwapa fursa kushindana vema.
Aidha alisema kuwa makabidhiano ya zawadi zilizoandaliwa kwa washindi
mbalimbali zitafanyika kwenye viwanja vya shule ya sekondari Popatlaly
mara baada ya kumalizika mashindano hayo.
Hata hivyo alisema kuwa mgeni rasmi katika mashindano hayo anatarajiwa
kuwa Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo,Dr.Fennela
Mukangara

No comments: