Thursday, July 9, 2015

TWIGA STARS YAPANGWA NA WENYEJI



Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Afrika (CAF) leo limetoa ratiba ya fainali ya michezo ya Afrika (All African Games), ambapo Timu ya Taifa ya Tanzania ya Wanawake (Twiga Stars) imepangwa kundi A pamoja na wenyeji Congo-Brazaville.


Katika droo iliyochezwa leo makao makuu ya CAF - Cairo na kupanga makundi ya fainali hizo za michezo ya Afrika, Tanzania imepangwa kundi A pamoja na wenyeji Congo - Brazaville, Nigeria na Ivory Coast, huku Kundi B likiwa na timu za Cameroon, Afrika Kusini, Ghana na Misri.

Kundi B lenye timu ya Twiga Stars linaonekana kuwa ndio kundi gumu zaidi kutokana na kuwa timu ya Nigeria, mabingwa mara mbili wa michuano hiyo, wenyeji Congo -Brazzavile washiriki mara mbili wa fainali hizo na timu ya Ivory Coast.

Twiga Stars ilifanikiwa kukata tiketi ya kucheza fainali hizo baada ya kuiondoa timu ya Taifa ya Zambia ya wanawake (She-Polopolo) kwa jumla ya mabao 6-5.

Fainali hizo za michezo ya Afrika zinatarajiwa kuanza kutimua vumbi nchini Congo - Brazzaville Septemba 3 - 18 mwaka huu.


IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF

No comments: