Saturday, October 24, 2015

DK. JOHN POMBE MAGUFULI AFUNGA KAZI MWANZA, AWAAMBIA WATANZANIA MKAGUSWE MIOYO YENU NA KUNIPIGIA KURA ZA NDIYO

????????????????????????????????????
 Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dk. John Pombe Magufuli akiingia kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza tayari kwa kuwahutubia maelfu ya wananchi waliojitokeza kwenye  mkutano wa ufungaji wa kampeni za CCM  uliofanyika uliofanyika jijini humo. 
Kesho oktoba 25 ndiyo siku ya upigaji kura kwa watanzania kumchagua kiongozi wanayemtaka na waliyeridhika na sera zake pamoja na Chama  kutokana na kampeni zilizofanywa kwa miezi miwili nchini kote huku vyama vikanadi sera zao japokuwa ni Chama cha Mapinduzi ndicho kilichochapisha ilani yake na kuzindua kitabu cha Ilani yake itakayotekelezwa kwa miaka mitano.
Dk John Pombe Magufuli akiwaomba kura wana Mwanza leo katika mkutano huo amewaombea kwa mungu ili wakawe na afya njema mpaka ifikapo keshi siku ya kupiga kura amewaambia kwamba Mungu akawaguse katika mioyo yenu ili mkanipigie kura niwe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Lakini pia mkawapigie wabunge wa CCM na Madiwani wa CCM ili Serikali yangu ya awamu ya tano   ikawajibike kwa tija kuwaletea maendeleo watanzania. Kwani mawasiliano ya kiutendaji katika maendeleo yatakuwa ni mazuri zaidi kuliko mkichagua wabunge na madiwani  wa upinzani ambao wanatoka nje ya vikao wakati wa kupitisha bajeti za maendeleo bungeni na katika mabaraza ya madiwani kwenye halmashauri.(PICHA NA JOHN BUKUKU-FULLSHANGWE-MWANZA)
????????????????????????????????????
????????????????????????????????????
Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dk. John Pombe Magufuli akiwapungia mikono wananchi waliojitokeza katika  mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
????????????????????????????????????
Wananchi wakimpokea Dk. John Pombe Magufuli hayupo pichani katika uwanja huo.
????????????????????????????????????
 Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dk. John Pombe Magufuli akielekea jukwaani mara baada ya kuwasili kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye uwanja wa CCM Kirumba.
????????????????????????????????????
Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dk. John Pombe Magufuli kulia akiwa na wagombea ubunge wa majimbo la Ilemela na Nyamagana kushoto ni Anjelina Mabula na Stanslaus Mabula kwenye mkutano huo wa kampeni.
????????????????????????????????????
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Kikwete akipungia wananchi mkono  wakati alipowasili kwenye uwanja wa CCM Kirumba.
????????????????????????????????????
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Kikwete akimnadi Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dk. John Pombe Magufuli kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
????????????????????????????????????
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Kikwete akiteta jambo na  Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dk. John Pombe Magufuli kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika CCM Kirumba jijini Mwanza.
????????????????????????????????????
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Kikwete na  Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dk. John Pombe Magufuli wakicheza kwa furaha nyimbo za hamasa za bendi ya TOT kwenye mkutano wa kufunga kampeni uliofanyika jijini Mwanza leo.
????????????????????????????????????
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Kikwete na  Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dk. John Pombe Magufuli pamoja na mgombea mweza Mama Samia Suluhu Hassan wakicheza nyimbo za hamasa kwenye mkutano wa kufunga kampeni uliofanyika jijini Mwanza.
????????????????????????????????????
Kundi la Yamoto Bandi likifanya vitu vyao jukwaani.
????????????????????????????????????
Kundi la Team Kibajaji lililoshiriki kikamilifu katika kampeni likimpigia debe Dk. John Pombe Magufuli.
????????????????????????????????????
Mwigizaji wa filamu Jacob Steven ambaye ni mmoja wa wanakikundi cha Team Kibajaji akizungumza katika mkutano huo jijini Mwanza.
????????????????????????????????????
Mbunge mtarajiwa viti maalum mkoa wa Tabora Irene Uwoya ambaye ni mmoja wa wasanii wa kundi la Team Kibajaji akimpigia debe Dk John Pombe Magufuli katika mkutano huo.
????????????????????????????????????
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mwanza na mjumbe wa Kamati ya Ushindi ya CCM Ndugu Anthony Dialo akimkaribisha Mratibu wa kampeni za Dk. John Pombe Magufuli Alhaji Abdallah Bulembo. 
????????????????????????????????????
Msanii Fid Q akifanya vitu vyake jukwaani wakati alipotumbuiza katika mkutano huo.
????????????????????????????????????
Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyuo vya Elimu ya Juu, Zainab Abdallah Issa akizungumza katika mkutano huo wa kufunga kampeni jijini Mwanza leo.
????????????????????????????????????
Mgombea Mwenza mama Samia Hassan Suluhu akiomba kura katika mkutano huo.
????????????????????????????????????
Kundi la wasanii waigizaji la Sema na Mwanao wakiwa jukwaani katika mkutano huo.
????????????????????????????????????
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Snura akitumbuiza katika mkutano huo wa kufunga kampeni.
????????????????????????????????????
????????????????????????????????????
Steve Nyerere akizungumza katika mkutano huo 
????????????????????????????????????
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Kikwete akihutubia mkutano wa kufunga kampeni jijini Mwanza leo.
????????????????????????????????????
Maelefu ya wananchi wakiwa katika mkutano huo.
????????????????????????????????????
????????????????????????????????????
????????????????????????????????????
 Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dk. John Pombe Magufuli akiwahutubia wananchi katika mkutano huo.
????????????????????????????????????
 Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dk. John Pombe Magufuli akisisitiza jambo wakati akiwahutubia wananchi hao  na kuwaomba kura za ndiyo siku ya uchaguzi kesho.
????????????????????????????????????
????????????????????????????????????
Kufuli la Magufuli kwa ajili ya kufunga kero za wananchi.
????????????????????????????????????
 Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dk. John Pombe Magufuli akizungumza katika mkutano huo huku Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Kikwete akimsikiliza kulia ni Mgombea mwenza mama Samia Suluhu Hassani.
????????????????????????????????????
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Kikwete akimnadi Mgombea Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli wa pili kutoka kulia, Mgombea Mwenza Mama Samia Hassan Suluhu na wagombea ubunge wa majimbo ya Ilemela Anjela Mabula wa kwanza kushoto  na Stanslaus Mabula Nyamagana wa tatu kutoka kushoto.
????????????????????????????????????
Mgombea urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli na Mgombea Ubunge Nyamagana Stanslaus Mabula wakiwa katika Picha ya kuchorwa.
????????????????????????????????????
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Kikwete aki akizungumza katika mkutano akizungumza jambo wakati akiwanadi Dk. John Pombe Magufuli kushoto, wagombea ubunge Stanslaus Mabula kulia na Anjela Mabula wa pili kutoka kushoto mgombea ubunge Nyamagana.

No comments: