Naibu katibu mkuu wa chama cha Democrasia na maendeleo CHADEMA Bwana SALUM MWALIMU akizungumza na wanahabari mapema leo Jijini Dar es salaam |
Chama cha Democrasia na
maendeleo CHADEMA pamoja na umoja wa katiba ya wananchi UKAWA wamesema kuwa upo
mpango unaoandaliwa na chama cha mapinduzi kwa kushirikiana na serikali
kuhakikisha kuwa wanakata mawasiliano hasa ya mtandao kwa siku ya upigaji kura Tanzania,mpango
ambao wamesema kuwa unasukwa kwa ajili ya kuhakikisha kuwa watanzania wanakuwa
hawana mawasiliano ya haraka kupenana habari za matokeo na uchaguzi kwa ujumla
siku hiyo.
Kauli ya kuhofia swala
hilo imetolewa leo mchana jijini Dar es salaam na kaimu katibu mkuu wa chama
cha CHADEMA Bwana SALUM MWALIMU ambapo amesema kuwa upo mpango wa kukata mawasiliano
ya data na internent kwa muda wa siku hiyo ambao amesema kuwa vikao vya kuamua
swala hilo vinaendelea huku akisema kuwa mpango huo unaweza kuvuruga uchaguzi
wa Tanzania.
Amesema kuwa mpango huo
ni mwendelezo wa vitisho na vihoja mbalimbali ambavyo vinafanywa na watawala
kuhakikisha kuwa wanashinda uchaguzi wa mwaka huu kwa njia yoyote ambapo
amewataka watanzania kuwa makini na kutotetereka kwa lolote kwani wako makini
kwa kila jambo linaloendelea katika uchaguzi hususani kipindi hiki cha kampeni
za lala salama.
Salum Mwalimu ambaye
pia ni mgombea ubunge wa jimbo la kikwajuni huko Zanzibar ameitaka mitandao ya
simu nchini kutokukubali kuingia katika siasa kwa njia hiyo kwani watakuwa
wamechangia kuvuruga uchaguzi huo.
Katika hatua nyingine Naibu
katibu mkuu huyo amesema kuwa chama chake pia kimenasa mipango mipya ya
watawala ambayo tayari vikao vimefanyika ya kuhakikisha kuwa vijana wa boda
boda katika maeneo mengi nchini wanakamatwa na kuwekwa ndani kwa muda hadi
uchaguzi upite ili kupunguza kura zao swala ambalo amesema kuwa lilipangwa
kuanza leo.
Amesema kuwa swala kama
hilo ni kukiuka haki za watanzania wanaotaka kufanya mabadiliko katika uchaguzi
wa mwaka huu jambo ambalo linaweza kuwasababishia matatizo makubwa kwa watawala mara baada ya uchaguzi mkuu.
Ikumbukwe kauli ya kukamatwa
kwa boda boda ilitolewa pia jana na mgombea urais wa UKAWA ndugu EDWARD LOWASA akiwa
katika kampeni huko tanga ambapo alisema kuwa wapo vijana kadhaa wa boda boda
ambao wamewekwa ndani bila makosa maalum huku akiwataka askari na vyombo vya
usalama kuacha kutumika kwa stail hiyo kwani kuna maisha baada ya uchaguzi na
wanaweza kujikuta matatizoni.
No comments:
Post a Comment